UWT Mwanza watoa msaada Sekou Toure, waahidi Mitano Tena kwa Rais Samia 2025
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa Mwanza Oktoba 11, 2021 umekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali ikiwemo sababuni, taulo za kike, vyandarua na mashuka katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza Sekou Toure ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Wiki ya UWT 2021.
Akizungumza wakati wa zoezi la kukabidhi mahitaji hayo, Mwenyekiti wa UWT Mkoa Mwanza, Hellen Bogohe amempongeza Rais Samia kwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo na uboreshaji wa sekta ya afya ikiwemo kutoa mashine ya CT Scan katika Hospitali ya Sekou Toure na kueleza kuwa zawadi watakayompa ni kumuongeza miaka tena katika uchaguzi wa mwaka 2025.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mahitaji mbalimbali ikwemo sabuni pamoja na taulo za kike yaliyokabidhiwa katika Hospitali ya Rufaa Sekou Toure kwa ajili ya kuwasaidia akina mama waliojifungua hospitalini hapo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya UWT 2021.
Tazama BMG TV hapa chini
SOMA>>> Habari zaidi kuhusiana na UWT
No comments: