LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kila mtu apambane na hali yake, usikubali mtu akutishe- Waziri Biteko

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Online Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko amewapa matumaini wachimbaji wa madini nchini baada ya kupiga marufuku tabia ya baadhi ya watumishi wasio waadilifu ambao wamekuwa wakiwapa vitisho ama kuwaomba rushwa wachimbaji kabla ya kuwahudumia.

Akizungumza Disemba 23, 2021 na wachimbaji madini katika machimbo ya Ntambalale Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Dkt. Biteko amesema Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan haiko tayari kuona wananchi wakionewa.

Aidha Dkt. Biteko amewataka wachimbaji na wafanyabiashara wa madini kufanya shughuli zao kwa kuzingatia sheria ikiwemo kulipa kodi kwani dhambi ya kukwepa kulipa kodi inaweza kusababisha mtu yeyote kuwatisha na wakatishika.

Katika hatua nyingine Waziri Dkt. Biteko amekagua shughuli mbalimbali katika mgodi wa Bulyanhulu na kuridhishwa na mabadiliko yanayofanyika mgodini hapo ikiwemo usimikaji wa mitambo ya uchimbaji madini inayoendeshwa kidigitali akisema hatua hiyo itafungua fursa zaidi ya ajira hususani kwa wanawake tofauti na ilivyo sasa ambapo wanaoendesha mitambo iliyopo kwa asilimia kubwa ni wanaume.

Aidha ameelekeza mgodi huo kushirikiana vyema na Halmashauri ya Msalala ili kuhakikisha fedha za CSR zinatekeleza miradi ya maendeleo inayoacha alama ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya elimu, afya na barabara. 
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Kwa mwaka 2021 mgodi wa Bulyanhulu umetenga zaidi ya shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya CSR.
Mgodi wa Bulyanhulu pia umeanza utekelezaji wa mpango wake wa kuhamia kwenye matumizi ya kidijitali katika kuendesha mitambo yake inayotumika kuchimba dhahabu.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko na viongozi mbalimbali walipotembelea mtambo wa kujenjua madini katika mgodi wa Bulyanhulu wilayani Kahama.
Msimamizi katika mgodi wa Bulyanhulu (katikati) akitoa ufafanuzi wa uendeshaji kwa Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko (kushoto) alipotembelea mgodini hapo.
Sehemu ya mwonekano wa mtambo wa kuchenjua dhahabu katika mgodi wa Bulyanhulu uliopo wilayani Kahama.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko (katikati) akiwasili katika mgosi wa Bulyanhulu.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa mgodi wa Bulyanhulu.
Wananchi na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko alipotembelea machimbo hayo.
Wananchi na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko alipotembelea machimbo hayo.
Wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Ntambalale wakiwasilisha kero zao mbele ya Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko (hayuko pichani) ambapo waliomba kero ya ukosefu wa vyoo katika machimbo hayo pamoja na ubovu wa barabara kushughulikiwa.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye mkutano huo.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Wachimbaji wakifuatilia mkutano huo.
Wachimbaji wakimsikiliza Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Viongozi mbalimbali wakifuatilia mkutano huo.
Wananchi wakifuatilia mkutano huo.
Wananchi wakifuatilia mkutano huo.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko alipotembelea machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko alipotembelea machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko akizungumza na viongozi katika alipotembelea machimbo ya Ntambalale wilayani Kahama.
Machimbo ya Ntambalale katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama.
Tazama BMG TV hapa chini

1 comment:

  1. To begin with, you don't have to worry about different gamers, as might be} playing in} for real money only against the home. Video poker is identified as|also called|also referred to as} a banking recreation for a similar cause. In most cases, a video poker recreation can be based mostly on a five-card draw version of the on line casino recreation. After you place your wager, might be} dealt five cards. You can take as much time as want to|you should|you have to} a glance at|have a glance at} them and decide which ones to maintain https://casino.edu.kg/1xbet-korea.html and which to discard. For every card you discard, you'll get a brand new} one from the deck.

    ReplyDelete

Powered by Blogger.