Baraza la UVCCM Nyamagana lampongeza Rais Samia
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Online Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, limepongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoiongoza vyema nchi pamoja na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa mwaka 2020/25.
Akisoma maazimio ya Baraza hilo kwenye kikao kilichofanyika Disemba 22, 2021. Katibu wa UVCCM Wilaya Nyamagana Malanyingi Matukuta alisema Rais Samia amekuwa kiongozi wa kuonesha dira ya Serikali anayoiongoza kwa kuzingatia uadilifu, utawala wa sheria, haki, usawa, mshikamano na kuimarisha demokrasia.
Alisema Rais Samia ametoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo miradi mipya na kuendeleza miradi iliyokuwepo.
Katibu wa
Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Nyamagana, Malanyingi
Matukuta (kulia) akisoma azimio la kumpongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa
utendaji kazi wake na kuiongoza nchi kwa weredi, wakati wa mkutano wa baraza la
umoja huo liliofanyika jijini Mwanza, kushoto ni Mwenyekiti wa umoja huo
Boniphace Zephania.
Mwenyekiti
wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Nyamagana Boniphace
Zephania(kushoto) akizungumza kabla ya kusomwa azimio la kumpongeza Rais wa Tanzania, Mhe. Samia
Suluhu Hassan kwa utendaji kazi wake na kuiongoza nchi kwa weredi, wakati wa
mkutano wa baraza la umoja huo liliofanyika jijini Mwanza, kulia ni katibu wa
umoja huo Malanyingi Matukuta.
Wajumbe wa Baraza la UVCCM Wilaya Nyamagana.
Soma hapa chini maazimio kamili ya Baraza la UVCCM Wilaya Nyamagana wakimpongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.
SOMA>>> Habari zaidi kuhusiana na UVCCM
No comments: