LIVE STREAM ADS

Header Ads

Dkt. Flora Lauwo aongoza Mahafali ya 22 Kidato cha Sita Mwanza Sekondari

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Online Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo amewaasa wadau mbalimbali wa elimu kushirikiana na Serikali kuboresha miundombinu ya elimu katika Shule ya Mwanza Sekondari hatua itakayosaidia kuinua zaidi ufaulu kwa wanafunzi.

Dkt. Laulo ametoa rai hiyo Machi 24, 2022 alipokuwa mgeni rasmi kwenye Mahafali ya 22 ya Kidato cha Sita yaliyofanyika shuleni hapo yakishirikisha wanafunzi 359 (wavulana 102 na wasichana 257) ambao wanatarajiwa kuhitimu masomo yao mwezi Mei mwaka huu 2022.

Amesema licha ya kazi nzuri inayofanywa na Serikali kupitia Rais Samia Suluhu Hassan ikiwemo ujenzi na ukarabati wa vyumba vya madarasa pamoja na nyumba za waalimu lakini bado kuna changamoto kwa wanafunzi wa kike kukosa chumba maalum kwa ajili ya kujistiri na kubadilisha taulo za kike wakati wa hedhi ambapo ametoa rai kwa wadau mbalimbali kusaidia kutatua changamoto hiyo.

Dkt. ametumia fursa hiyo kukabidhi taulo za kike kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wa kike shuleni hapo pamoja na kukabidhi jezi za michezo kwa ajili ya wavulana na wasichana shuleni hapo ikiwa ni sehemu ya taasisi yake kwa kushirikiana na wadau wengine ikiwemo taasisi ya 'The Desk & Chair Foundation' kuhamaisha michezo mashuleni.

Naye Mkuu wa Shule ya Mwanza Sekondari, Mwl. Sudi Gewa ameishukuru Serikali kwa uamuziwake wa kuzikarabati Shule kongwe nchini ikiwemo Shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 1959 ambayo kwa sasa wanafunzi wote wa kike wa kidato cha tano na sita wanaishi bweni. Aidha amepongeza uamuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan wa kuruhusu wanafunzi waliopata ujauzito kurejea shuleni ambapo Shuleni hadisasa imepokea wanafunzi wawili ambao wameahidi kusoma kwa bidii huku wakijutia waliyopitia.

Katika hatua nyingine Mwl. Gewa amebainisha kuwa shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vyombo vya kukusanyia uchafu na kuupeleka dampo na kuomba wadau kusaidia upatikanaji wa vifaa hivyo ikiwemo bajaji ili kuwaondolea gharama kubwa zinazohitajika kuwalipa wazabuni wa kuzoa uchafu ambazo ni kati ya shilingi laki saba hadi laki tisa kwa mwenzi.

Awali akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wenzake, Scholastica Nchehe alisema Shule ya Mwanza Sekondari inakabiliwa na uhaba wa vifaa vya maabara na kuomba wadau wa elimu na Serikali kushirikiana kutatua changamoto hiyo ili kuwasaidia wanafunzi kujifunza vyema.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG 
Mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo akizungumza kwenye Mahafali hayo ambapo pamoja na mambo mengine pia amewahimiza wahitimu kutumia mitandao ya kijamii kwa tija kama anavyofanya yeye kwenye shughuli zake za kuisaidia jamii badala ya kutumia mitandao hiyo kwenye masuala ya 'udaku'.
Wanahabari (kulia) wakinasa matukio kwenye mahafali hayo wakati mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo (kushoto) akizungumza.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo (kushoto) amekabidhi jezi za michezo kwa ajili ya timu ya Netball pamoja na taulo za kike kwa ajili ya wanafunzi wa Shule ya Mwanza Sekondari.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo (kulia) akikabidhi taulo za kike kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya Mwanza Sekondari ambapo taulo hizo zimetolewa na taasisi hiyo kwa kushirikiana na wadau wengine.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo (kushoto) akikabidhi vyeti kwa wanafunzi wa kidato cha sita Mwanza Sekondari wanaotarajiwa kuhitimu masomo yao mwezi Mei mwaka huu 2022.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo (kushoto) akikabidhi vyeti kwa wanafunzi wa kidato cha sita Mwanza Sekondari wanaotarajiwa kuhitimu masomo yao mwezi Mei mwaka huu 2022.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo (kushoto) akikabidhi vyeti kwa wanafunzi wa kidato cha sita Mwanza Sekondari wanaotarajiwa kuhitimu masomo yao mwezi Mei mwaka huu 2022.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo (kushoto) akikabidhi vyeti kwa wanafunzi wa kidato cha sita Mwanza Sekondari wanaotarajiwa kuhitimu masomo yao mwezi Mei mwaka huu 2022.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo (kushoto) akikabidhi vyeti kwa wanafunzi wa kidato cha sita Mwanza Sekondari wanaotarajiwa kuhitimu masomo yao mwezi Mei mwaka huu 2022.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo (kushoto) akikabidhi vyeti kwa wanafunzi wa kidato cha sita Mwanza Sekondari wanaotarajiwa kuhitimu masomo yao mwezi Mei mwaka huu 2022.
Mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo pia alikabidhi zawadi kwa waalimu wa wanafunzi wa kidato cha sita waliofanya vizuri katika mitihani yao ya majaribio.
Mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee (Nitetee Foundation) ya jijini Mwanza, Dkt. Flora Lauwo pia alikabidhi zawadi kwa waalimu wa wanafunzi wa kidato cha sita waliofanya vizuri katika mitihani yao ya majaribio.
Wanafunzi 359 (wavulana 102 na wasichana 257) katika Shule ya Mwanza Sekondari wanatarajiwa kuhitimu kidato cha sita mwaka huu 2022.
Wanafunzi wa kidato cha sita (kulia) wanaotarajiwa kuhitimu masomo yao mwezi Mei mwaka huu 2022 katika Shule ya Mwanza Sekondari wakiwa kwenye mahafali yao. Kushoto ni wazazi na walikwa mbalimbali kwenye mahafali hayo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Mwanza Sekondari, Debora Ringo amewaasa wanafunzi wa kidato cha sita wanaotarajiwa kuhimu mwezi Mei mwaka huu 2022 kuzingatia kile walichojifunza na kufanya vyema kwenye mtihani wao ili kutimiza ahadi waliyoitoa ya kufaulu kwa daraja la kwanza zaidi ya 200.

No comments:

Powered by Blogger.