LIVE STREAM ADS

Header Ads

Serikali yatoa Bilioni 93.1 kutekeleza miradi ya maendeleo Iringa

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Online Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Miradi ya maendeleo yenye thamani ya Jumla ya sh. 93.1 bilioni imetekelezwa katika Wilaya ya Iringa Kwa kipindi Cha mwaka mmoja tangu Serikali ya Awamu ya Sita ilipoingia madarakani.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Moyo akizungumza na wazee pamoja na viongozi wa dini wa Wilaya hiyo mkoani Iringa alisema kiasi hicho cha fedha kilielekezwa katika miradi mbalimbali ikiwemo ya afya, elimu, miundombinu ya barabara, maji na umeme.

Katika kikao hicho Mkuu wa Wilaya alisema Serikali iliyochini ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha wazee wanapata unafuu wa matibabu bure jumla ya wazee 793 wamepatiwa vitambulisho ili kuwaondoshea changamoto ya matibabu.

Moyo alisema kuwa Shilingi 93.1 bilioni zimetumika katika miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Iringa ikiwemo ujenzi wa barabara ya Kihesa Kilolo – Igumbilo itakayosaidia kupunguza msongamano wa magari mjini.

Alisema kwa sasa magari yote yanapita katikati ya mji na kusababisha msongamano mkubwa kutokana na ukosefu wa barabara mbadala.

“Ikitokea roli likapata ajali mlima wa Ipogoro na kuziba barabara hali lazima iwe tete, lakini Serikali imetoa Sh7.75 bilioni kwa ajili ujenzi wa barabara hii” alisema.
Moyo alisema shughuli zinazofanyika kwa sasa ni ujenzi wa madaraja na barabara kwa mita 450.
Moyo alisema fedha nyingine zimetumika kwenye kuboresha miradi ya elimu, afya, ujenzi wa uwanja wa ndege, machinjio ya kisasa, sekta ya umeme na biashara.

Aidha mkuu wa wilaya ya IringaMohamed Hassan Moyo alisema kuwa katika sekta ya afya walipata zaidi ya bilioni 5 ambazo zimetumika katika ujenzi ujenzi wa Hospitali,vituo vya afya na zahanati.

Alisema kuwa kiasi cha zaidi ya bilioni mbili zilitumika katika sekta ya elimu msingi kwenye ujenzi wa madarasa,ofisi za walimu,nyumba za walimu na vyoo wakati zaidi ya kiasi cha bilioni 4 zilitumika katika kuboresha miundombinu ya majengo ya shule za sekondari ambapo walitumia katika ujenzi wa madarasa,ofisi za walimu,nyumba za walimu na vyoo.

Moyo alisema kuwa mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania samia Suluhu Hassan ameboresha sekta zote katika wilaya ya Iringa ambapo ametoa kiasi bilioni 93.1 katika sekta za afya, elimu, maendeleo ya jamii, maji, umeme, biashara na mapato, usafiri, ujenzi na barabara

Alisema kuwa kwa kiasi kikubwa fedha hizo zimechochea ukuaji wa uchumi na kuleta maendeleo kwa wananchi wa wilaya ya Iringa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Manispaa ya Iringa, Said Rubeya alisema kazi zilizofanyika zitasaidia kuongeza kasi ya maendeleo kwenye mji huo.

“Tunaona kwa macho kazi zilizofanyika, niipongeze Serikali lakini nikupongeze mkuu wa wilaya kwa kuzungumza haya mbele ya wazee. Vijana wanaweza kukimbia lakini wazee wanaijua njia, tuwasikilize” alisema.

Kazi kubwa Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa akiifanya ndani na mwaka mmoja amefanya mambo mengi Sana na akija Iringa tutampongeza tena-Said Rubeya Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Iringa mjini

No comments:

Powered by Blogger.