LIVE STREAM ADS

Header Ads

DC Iramba aguswa na adha ya wananchi wa Kijiji cha Msai kukosa Zahanati

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda (katikati) akishiriki kufyatua matofali wakati wa mfululizo wa ziara yake ya kikazi ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo aliyoifanya Kata ya Shelui na Mtoa wilayani humo jana May 29, 2023 akiwa ameongoza na wataalam, watendaji wa Kata na Tarafa pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama.

Na Mwandishi Wetu, Iramba
Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amesema atafanya mawasiliano na wahusika wa sekta ya afya ili ziweze kupatika fedha za kumalizia ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Msai

Kupatikana kwa fedha hizo na kukamilika kwa ujenzi wa zahanati hiyo kutawaondolea adha wananchi ya kutembea umbali mrefu kwenda kupata huduma za matibabu maemo mengine.

Mwenda ameyasema hayo wakati alipokuwa kwenye ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika Kata yaMtoa na Shelui pamojana kusikiliza kero za wananchi ili kuzitafutia ufumbuzi.

Akiwa katika Zahanati ya Msai inayojengwa kwa nguvu za wananchi wakisaidiwa na fedha za Mfuko wa Jimbo zinazo simamiwa na Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi Dkt. Mwigulu Nchemba aliombwa na wananchi kupatikana kwa fedha za kumalizia ujenzi wa jengo hilo la zahanati hiyo Ili ianze kutoa huduma na kuwaondolea kero wakazi wa kijiji hicho hasa Wajawazito na watoto.

"Nimesikia maombi yenu napenda kuwasiliana na wahusika ili kuwaomba tupate fedha za kumalizia ujenzi wa zahanati iweze kukamilika na kuanza kutoa huduma haraka iwezekanavyo," alisema Mwenda.

Alisema kijiji hicho ni kikubwa na kuna wananchi wengi lazima ujenzi wa zahanati hiyo ukamilike haraka ili wananchi wasiendelee kwenda mbali kupata huduma za afya.

Aidha,Mwenda akiwa kwenye ziara hiyo aliwasisitiza wasimamizi wa miradi yote inayotekelezwa katika wilaya hiyo kuhakikisha inakamilika kabla ya June 10,2023.

Katika hatua nyingine Mwenda amewaomba wananchi kuendelea kujitolea nguvu kazi kwa kushirikiana na wataalam na viongozi katika kutekeleza miradi yote inayofadhiliwa na serikali na kuhakikisha inamalizika kwa wakati na viwango kulingana na thamani ya fedha walizozipokea
Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda, akipokea taarifa wakati wa ziara hiyo.
Kazi za utekelezaji wa miradi zikiendelea.
Ziara ikiendelea.
Ziara ikiendelea.

No comments:

Powered by Blogger.