LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kiota cha burudani 'A2C Bar & Grill' kuzinduliwa jijini Mwanza

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
 
Baada ya kiota cha burudani 'The Kiss Club' kilichopo Kirumba jijini Mwanza kufungwa kwa muda, sasa kinarudi upya ambapo ukarabati wake uko katika hatua za mwisho kukamilika ili kukata kiu ya wapenda burudani.

Kiota hicho, The Kiss Club kwa sasa kitajulikana kama A2C Bar & Grill ambapo kitakuwa na huduma mbalimbali ikiwemo vinywaji na chakula kitamu bila kusahau muziki mzuri.

Kwa mjibu wa Mkurugenzi wa A2C, Benedict Mara, uzinduzi wa kiota hicho cha burudani unatarajiwa kufanyika Ijumaa Julai 14, 2023.
Tazama picha zaidi hapa chini.

No comments:

Powered by Blogger.