LIVE STREAM ADS

Header Ads

Barrick North Mara Runners Club kushiriki mbio za Capetown Marathon 2023

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Baadhi ya wakimbiaji wa klabu ya Barrick North Mara Runners Club wakifurahi baada ya kumaliza kushiriki kukimbia katika mbio za Lake Victoria Marathon zilizofanyika jijini Mwanza hivi karibuni.
Baadhi ya wakimbiaji wa klabu ya Barrick North Mara Runners Club wakifurahi baada ya kumaliza kushiriki kukimbia katika mbio za Lake Victoria Marathon zilizofanyika jijini Mwanza hivi karibuni.
Baadhi ya wakimbiaji wa klabu ya Barrick North Mara Runners Club wakifurahi baada ya kumaliza kushiriki kukimbia katika mbio za Lake Victoria Marathon zilizofanyika jijini Mwanza hivi karibuni.
Baadhi ya wakimbiaji wa klabu ya Barrick North Mara Runners Club wakifurahi baada ya kumaliza kushiriki kukimbia katika mbio za Capital City Marathon zilizofanyika jijini Dodoma hivi karibuni.
Kapteni wa timu ya Barrick North Mara Runners Club,Sarah Cyprian (mwenye Tshirt ya bluu) akitimka mbio wakati wa mashindano ya Lake Victoria Marathon zilizofanyika jijini Mwanza karibuni ambao aliibuka mshindi wa 4 katika mbio za kilometa 21 kwa upande wa Wanawake.


****
Wakati mchezo wa mashindano ya riadha yanazidi kuwa na mwamko mkubwa nchini, yakijumuisha watu wenye umri wa rika mbalimbali, klabu mbalimbali za marathon zimezidi kuanzishwa na baadhi yake zinazidi kuwa tishio katika mashindano mbalimbali kutokana na kuwa na wachezaji wenye vipaji vikubwa.

Barrick North Mara Runners Club, inayoundwa na wafanyakazi wa mgodi wa Barrick wa North Mara, ni moja ya timu ambayo inazidi kuja juu kwa kasi ambapo kwa sasa ipo kwenye maandalizi ya kwenda kushiriki, Capetown Marathon ya umbali wa kilometa 42. Mashindano ya mbio hizi yanatarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu nchini Afrika kusini.

Katika mahojiano na kapteni wa timu hiyo Sarah Cyprian karibuni, alisema timu hiyo ilianzishwa mwaka 2016 na inajumuisha wakimbiaji 66, miongoni mwao wanaume wapo 53 na Wanawake 13.

Alisema baadhi ya mashindano ambayo klabu hiyo imeshiriki ameyataja kuwa ni Kilimanjaro International Marathon -Moshi, Capital City Marathon -Dodoma(ilitoa mshindi wa tisa wa umbali wa kilometa 21 ) , Serengeti Migration marathon 21km-Mugumu, Serengeti Safari Marathon 21km-Lamadi na Lake Victoria Marathon -Mwanza (ilitoa mshindi wa 4 kwa wanawake umbali wa kilometa 21).

Mashindano makubwa ambayo timu hiyo imeshiriki na kung’ara ameyataja kuwa ni Kilimanjaro International Marathon ambapo ilishiriki mbio za kilometa 21 na kilometa 42.Kwa mbio hizo za masafa marefu ya kilometa 42 klabu iliwakilishwa na yeye mwenyewe. (Sarah Cyprian).

Akielezea siri ya mafanikio ya klabu Sarah alisema “Kampuni ya Barrick inayo sera mathubuti katika kusaidia wafanyakazi kwenye upande wa michezo. Kwanza kwa kuwa na miundo mbinu ya mazoezi kama gym, swimming pool, uwanja wa mpira wa miguu , uwanja wa mpira wa kikapu pamoja na uwanja wa mpira wa pete. Pia inatoa vifaa na nyenzo mbalimbali za kufanyia mazoezi,vilevile kugharamia huduma zote tunapoenda kwenye mashindano nje”.

Aliongeza kusema kuwa Kampuni pia kupitia kitengo cha Afya na Usalama huwa inaandaa mashindano ya ndani kwa kushindanisha idara mbali mbali hii ni kama njia moja wapo yakuweza kuweka vizuri afya za mwili na akili za wafanyakazi wawapo kazini.

Kuhusu ni jinsi gani wanaweza kutenga muda wa kazi na muda wa kufanya mazoezi Sarah alisema “ Kila mtu ana masaaa 24 katika siku.Klabu ya North Mara Runners huwa tunatenga muda wa saa moja katika siku kufanya mazoezi.Mazoezi hayo huwa tunafanya jioni mara baada ya kutoka kazini,na mara chache ratiba zinapokuwa zinabana jioni huwa tunafanya mazoezi saa kumi alfajiri kabla ya kwenda kazini”.

Kuhusiana na changamoto wanazokutana nazo katika mazoezi na kushiriki mashindano alisema kulingana na majukumu ya kazi huwa kuna wakati ni vigumu wote kwenda kushiriki mashindano, lakini huwa wanajitahidi kutoa wawakilishi kwa ajili ya kushiriki mashindano, na kampuni huwa inawaunga mkono wakati wote.

Akitoa maoni kuhusu maendeleo ya tasnia ya mchezo wa mbio za marathon nchini alisema katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na mwitiko mkubwa katika mchezo wa mbio na kushauri kuwa ni vizuri kuanza maandalizi mapema kwa vijana wadogo ili kuweza kuwa na washiriki wengi katika mbio za kimataifa.Aliongeza kusema kuwa kuna wakimbiaji wengi wenye vipaji nchini kwa sasa ambao wanashiriki mashindano ya marathon mbalimbali yanayoandaliwa nchini.

Sarah alitoa wito kwa jamii kujitahidi kutenga muda hata nusu saa kwa siku kufanya mazoezi. “Mazoezi yanasaidia kuimarisha afya ya akili na mwili. Pia mazoezi yanasaidia kuweza kujikinga na magonjwa yasioambukiza kama kisukari, shinikizo la damu na unene wa kupindukia”alisema.

Kuhusu malengo ya baadaye ya klabu hiyo alisema “Kauli mbiu ya club yetu ni ‘We run for fun and healthy’ hivyo basi bado tunajukumu la kuhimiza wafanyakazi wengi zaidi kufanya mazoezi kwa ajili ya afya zetu, kwani mazoezi pia yamekuwa yakituweka vizuri kiakili hata kuweza kutimiza majukumu yetu kazini kwa ufanisi zaidi.Lakini pia kuweza kushiriki zaidi katika marathoni za kimataifa.”

No comments:

Powered by Blogger.