LIVE STREAM ADS

Header Ads

Shamba la kwanza la Vanilla Kanda ya Ziwa lazinduliwa

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Mkurugenzi Mwanzilishi wa Makampuni ya Vanilla International Limited, Simon Mnkondya akionesha zao la Vanilla katika Shamba kubwa la Kilimo cha Vanilla kwa njia za kisasa katika Kijiji cha Nyamikoma kata ya Mwamashimba wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
***

Kampuni ya Vanilla International Limited imezindua Shamba kubwa la Kilimo cha Vanilla kwa njia za kisasa Kanda ya Ziwa katika Kijiji cha Nyamikoma kata ya Mwamashimba wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo leo Jumanne Julai 4,2023 Mkurugenzi Mwanzilishi wa Makampuni ya Vanilla International Limited, Simon Mnkondya amesema katika shamba hilo la Vanilla lenye ukubwa wa hekari tatu wanategemea kupata Kilo 6000 za Vanilla kila mwaka zenye thamani ya zaidi ya Dola Milioni 2.5 kwa soko la kimataifa sawa na takribani Shilingi Bilioni 6 za Kitanzania.

“Mazao ya Vanilla katika shamba hili yamestawi kwa ustawi kwa ubora kwa sababu ya upatikanaji wa unyevu hewa wa asilimia 85% ( Humidity 85%) ambayo ni (hali ya hewa wezeshi) mazingira wezeshi ya kilimo cha Vanilla ambayo tumeitengeneza kwa kutumia umwagiliaji wa njia ya bunduki”,ameeleza Mnkondya ambaye pia Mwanzilishi wa mashamba makubwa ya kilimo cha Vanilla (Vanilla Village) yaliyopo Zanzibar, Arusha, Dodoma na Mwanza.

“Katika huu mradi ambalo ndiyo shamba kubwa Kanda ya Ziwa ambalo limelimwa kwa njia ya Mashamba kitalu/mashamba ya mahema (Green Houses). Shamba hili limetoa vanilla ambayo ni ndefu kuliko vanilla zote duniani na kuvunja rekodi ya kuwa na mita 10 kwa urefu”,ameongeza Mnkondya.

Amesema Vanilla zilizolimwa kwenye shamba hilo ni vanilla ambazo zimewahi kuzaa kuliko vanilla zote za Kanda ya Ziwa kwani zimezaa ndani ya miezi saba.

Akifafanua Zaidi amesema shamba hilo la Vanilla lilikuwa ni nusu jangwa ambapo kwa kutumia mifumo ya maji ya kisasa za Umwagiliaji wa matone na Umwagiliaji wa bunduki (Rain gun)’ umefanya hilo eneo la jangwa kutoka kuwa kavu mpaka eneo la kijani.

“Hii imetokana na kwamba tumefunika shamba kwa kutumia vifaa vinavyokata mionzi ya jua kwa asilimia 55% na hivyo kutengeneza kivuli cha 55% hali iliyosababisha mimea isiathiriwe na jua.
Katika eneo hili kulikuwa na upepo mkali ambapo tumekata upepo huo kwa kutumia vyandarua kivuli (shade net)”,amesema Mnkondya.
Mkurugenzi Mwanzilishi wa Makampuni ya Vanilla International Limited, Simon Mnkondya akiwa kwenye Shamba la Vanilla.

“Eneo hili lilikuwa na vumbi jingi linalotoka kwenye machimbo ya dhahabu, hilo vumbi limekatishwa kwa kutumia vyandarua vivuli. Vumbi hili lingeathiri mimea kwa kuziba matundu hewa (stomatas) ambayo inatumika kwa ajili ya kutoa hewa ukaa na Oksijeni”,ameeleza.

Amebainisha kuwa kutokana na ukubwa wa bei ya Vanilla ambalo ni zao la pili kwa bei duniani inayofikia dola 430 kwa kilo moja sawa na shilingi Milioni ya Tanzania, wananchi wengi wa Kanda ya Ziwa na nchi kwa ujumla wamefika hilo kutembelea shamba hilo na kuhamasika kulima zao la Vanilla.

“Kampuni yetu ya Vanilla International imeweza kujitwalia wawekezaji (wakulima) wa zao la Vanilla kufikia 1350 nchi nzima ambapo kabla ya uhamasishaji huo wawekezaji wa zao la Vanilla walikuwa hawafiki 50.Mwanza hapakuwa na hata mkulima mmoja sasa hivi wanazidi 12 ambao wote wamejifunza kwenye shamba letu la Kwimba”,amesema.

Ameongeza kuwa zao la Vanilla ni zao lenye bei kubwa kuliko Silver (fedha) na linachuana na dhahabu na hivyo kufanya wachimbaji wa dhahabu Kanda ya Ziwa kuanza kujikita kwenye zao la Vanilla kama ilivyo kwa Dkt. Daniel Mrema wa Nyamikoma Mwanza ambaye ameanza kilimo hicho.

Kampuni hiyo pia imezindua Namba za Simu 0624300200 na 0769300200 kwa ajili ya kufundishia wananchi bure Kanda ya Ziwa kuhusu Kilimo cha Vanilla. Kupitia namba hizo mwananchi anaweza kutumia lugha yoyote ikiwemo Kisukuma, Kihaya. nk kupata huduma juu ya kilimo cha Vanilla.

“Kampuni yetu ya Vanilla International Limited inakukaribisha kuwekeza katika kilimo cha vanilla chenye uwezo mkubwa wa kukuinua kiuchumi. Zao la vanilla linaanza kuvunwa baada ya miezi 7(vikonyo) na mwaka 1 (matunda) lakini unavuna kwa miaka 60. Ukilima vanilla nasi utanufaika wewe,watoto na wajukuu. kwa sasa bei ya kilo moja ni 1,000,000/= na baada ya miaka 6 itakuwa 3,000,000/= kwa kilo ya vanilla. Soko la vanilla liko Dubai na dunia nzima”,ameeleza.
Mkurugenzi Mwanzilishi wa Makampuni ya Vanilla International Limited, Simon Mnkondya akionesha zao la Vanilla wakati akizindua Shamba kubwa la Kilimo cha Vanilla kwa njia za kisasa katika Kijiji cha Nyamikoma kata ya Mwamashimba wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Muonekano wa sehemu ya Shamba kubwa la Kilimo cha Vanilla kwa njia za kisasa katika Kijiji cha Nyamikoma kata ya Mwamashimba wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Muonekano wa sehemu ya Shamba kubwa la Kilimo cha Vanilla kwa njia za kisasa katika Kijiji cha Nyamikoma kata ya Mwamashimba wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Muonekano wa sehemu ya Shamba kubwa la Kilimo cha Vanilla kwa njia za kisasa katika Kijiji cha Nyamikoma kata ya Mwamashimba wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Mkurugenzi Mwanzilishi wa Makampuni ya Vanilla International Limited, Simon Mnkondya akionesha zao la Vanilla wakati akizindua Shamba kubwa la Kilimo cha Vanilla kwa njia za kisasa katika Kijiji cha Nyamikoma kata ya Mwamashimba wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Mkurugenzi Mwanzilishi wa Makampuni ya Vanilla International Limited, Simon Mnkondya akiwa kwenye Shamba kubwa la Kilimo cha Vanilla kwa njia za kisasa katika Kijiji cha Nyamikoma kata ya Mwamashimba wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Na Malunde Blog

No comments:

Powered by Blogger.