LIVE STREAM ADS

Header Ads

Barrick North Mara Runners washiriki mbio za Transec Lake Victoria Marathon Mwanza

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakijiandaa kuanza kukimbia mbio hizo zilizofanyika Jumapili Julai 02, 2023 jijini Mwanza kwa umbali wa KM 05, KM 10 na KM 21.


Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wameshiriki mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon 2023 zilizofanyika msimu wa tatu Julai 02, 2023 katika viunga vya Jiji la Mwanza.

Wafanyakazi hao wanaounda kikundi cha Barrick North Mara Runners wamesema mbali na kuimarisha kujiimarisha kimwili na kiafya pia ushiriki wa michezo mbalimbali ikiwemo mbio hizo unawazaidia kuimarisha mahusiano kazini.

“Lengo letu ni kujiweka sawa kimwili na kiafya ili kuondokana na msongo wa mawazo kazini ambapo uongozi wa mgodi umekuwa ukiwasaidia waajiriwa kujijenga kiafya ili kutimiza vyema majukumu yao” alisema Katibu wa Barrick North Mara Runners, Sarah Cyprian.

Naye Mratibu wa mbio za Transac Lake Victoria Marathon, Frank alisema mbio hizo zimelenga kutangaza vivutio vya utalii jijini Mwanza, kuhamasisha utunzaji wa mazingira hususani katika Ziwa Victoria pamoja na kusaidia jamii yenye uhitaji ambapo kwa mwaka huu watachangia shilingi milioni tano kwa ajili ya matibabu ya watoto katika hospitali ya rufaa Bugando.

Kwa upande wake mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Hassan Masala akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mwanza Amos Makalla alisema mbio hizo zina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa jiji la Mwanza kupitia huduma mbalimbali walizopata washiriki zaidi ya 1,500.
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakishiriki mbio hizo zenye lengo la kutangaza vivutio vya utalii jijini Mwanza, kutunza mazingira ya Ziwa Victoria pamoja na kusaidia watoto wanaotibiwa Saratani katika Hospitali ya Kanda Budando.
Mwenyekiti wa kikundi cha wafanyakazi wanariadha cha Barrick North Mara Runners, Emmanuel Nyinyimbe (kulia) akishiriki mbio za Transec Lake Victoria Marathon 2023 umbali wa kilomita 21.
Mwenyekiti wa kikundi cha wafanyakazi wanariadha cha Barrick North Mara Runners, Emmanuel Nyinyimbe (kulia) akishiriki mbio za Transec Lake Victoria Marathon 2023 umbali wa kilomita 21.
Washiriki wa mbio za Transec Lake Victoria Marathon 2023 akiwemo Katibu wa Barrick North Mara Runners, Sarah Cyprian (mwenye kofia) aliyemaliza nafasi ya nne umbali wa kilomita 21.
Washiriki wa mbio za Transec Lake Victoria Marathon 2023 akiwemo Katibu wa Barrick North Mara Runners, Sarah Cyprian (wa pili kushoto) aliyemaliza nafasi ya nne umbali wa kilomita 21.
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiendelea kukata upepo umbali wa kilomita 21.
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiendelea kukata upepo umbali wa kilomita 21.
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiendelea kukata upepo umbali wa kilomita 21.
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiendelea kukata upepo umbali wa kilomita 21.
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiendelea kukata upepo umbali wa kilomita 21.
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwasili katika eneo la 'Finish' baada ya kumaliza mbio za kilomita 10 na kilomita 21.
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwasili katika eneo la 'Finish' baada ya kumaliza mbio za kilomita 10 na kilomita 21.
Washiriki wa mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon wakiwemo wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwasili katika eneo la 'Finish' baada ya kumaliza mbio za kilomita 10 na kilomita 21.
Wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwa kwenye mbio za riadha za Transec Lake Victoria Marathon msimu wa tatu zilizofanyika jijini Mwanza Julai 02, 2023.
Katibu wa Barrick North Mara, Sarah Cyprian (kushoto) akipokea zawadi ya cheti na fedha taslimu baada ya kumaliza nafasi ya nne umbali wa kilomita 21 kwenye mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023.
Katibu wa Barrick North Mara, Sarah Cyprian akifurahia baada ya kumaliza nafasi ya nne umbali wa kilomita 21 kwenye mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023 jijini Mwanza.
Wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kushiriki mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023 jijini Mwanza.
Wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kushiriki mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023 jijini Mwanza.
Wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kushiriki mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023 jijini Mwanza.
Wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kushiriki mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023 jijini Mwanza.
Wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kushiriki mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023 jijini Mwanza.
Wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wengine wa mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023 jijini Mwanza.
Wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wengine wa mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023 jijini Mwanza.
Washindi wa mbio za Transac Lake Victoria Marathon 2023 akiwemo Katibu wa Barrick North Mara Runners, Sarah Cyprian (wa pili kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali akiwemo mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Hassan Masala (wa pili kulia waliosimama).
SOMA PIA>>> Habari zaidi hapa

No comments:

Powered by Blogger.