LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wataalam sekta ya afya Babati watoa changamoto zao kwa Mbunge Gekul, Wanufaika wa TASAF nao waibuka

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com

Mmoja wa Wataalam wa Sekta ya Afya Hospitali ya Mji Babati mkoani Manyara akielezea changamoto walizonazo mbele ya Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini, Pauline Gekul (hayupo pichani) wakati wa ziara yake ya kusikiliza kero na kuzitafutia ufumbuzi.

...............................................

Na Mwandishi Wetu, Babati

WATAALAM wa Afya wa Hospital ya Mji Babati mkoani Manyara wametoa malalamiko yao kwa Mbunge wa Jimbo la Babati Mji Pauline Gekul kutokana na changamoto wanazozipitia kwenye masuala  ya kiutumishi.

Wataalam hao wametoa malalamiko hayo baada ya kukutana na mbunge huyo katika ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi, ziara ambayo anaifanya jimbo jimbo lote baada ya kumalizika kwa vikao vya bunge la bajeti hivi karibuni.

Baadhi ya malalamiko waliolalamikia ni ufinyu wa kikokoteo baada ya kustaafu, kutopandishiwa mishahara baada ya kumaliza masomo Yao pindi wakiwa Kazini pamoja na kucheleweshewa kwa pindi wanapohamishwa vituo vya kazi.

Hivyo wamemuomba Mbunge huyo kupelekea malalamiko yao Bungeni ama kwa Waziri husika ili wajue namna ya kutatua changamoto zao.

"Nilikuwa sijui kuhusu changamoto hii nitazifikisha kwa wahusika naamini ndani ya muda zitafanyiwa kazi kwani ni jambo la kitaifa," alisema Gekul.

Wakati huo huo wakazi wa Mtaa wa Dawari Kata ya Bonga wameilalamikia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa kutowalipa fidia zao ndani ya miezi mitatu baada ya kufanya kazi walizopangiwa kufanya ili kujikimu na kimaisha.

Malalamiko hayo yamekuja mara baada ya Mbunge wa Jimbo la Babati Mji Pauline Gekul kufanya ziara katika Kata hiyo ikiwa na lengo la kusikiliza na kutatua Kero za wananchi

Akitoa ufafanuzi juu ya malalamiko hayo Mkuu wa Idara ya TASAF wa Halmashauri ya Mji Babati, Esther alikiri kuwepo kwa malalamiko hayo lakini malipo yao yameshindwa kukamilika kutokana na baadhi yao kufanya kazi nje na utaratibu na kuwa fedha za ruzuki ziko pale pale kwa wale ambao wamekithi vigezo  vya kufanya kazi za kijamii.

Watumishi hao wa Sekta ya Afya wakiwa kwenye mkutano huo wa Mbunge wa kusikiliza kero.
Kero zikiendelea kusikilizwa.
Kero zikitolewa. 

No comments:

Powered by Blogger.