LIVE STREAM ADS

Header Ads

TANESCO yakutana na madiwani Manispaa ya Shinyanga

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Leo Mwakatobe akizungumza kwenye kikao cha TANESCO na Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Johari Samizi akizungumza wakati akifungua Kikao cha TANESCO na Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Shinyanga limefanya kikao na madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya kuimarisha mahusiano na mawasiliano ili kupunguza malalamiko mbalimbali kutoka kwa wananchi.

Kikao hicho chenye kauli mbiu ‘TANESCO Yetu, Umeme Wetu, Njoo Tuzungumze’ kimefanyika leo Jumatano Novemba 15,2023 katika ukumbi wa Karena Hotel Mjini Shinyanga ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Johari Samizi.

Katika kikao hicho, madiwani wameeleza changamoto walizonazo kwenye maeneo yao pamoja na vipaumbele vya maeneo yanayopaswa kupatiwa huduma ya umeme.

Akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Johari Samizi ameipongeza TANESCO kwa kufungua milango ya kukutana na Madiwani ambao ni wawakilishi wa wananchi akibainisha kuwa mazungumzo yanaleta hitimisho la mambo yote.

“Kauli mbiu hii ya TANESCO Yetu, Umeme Wetu, Njoo Tuzungumze ni nzuri kwani, hitimisho la mambo yote ni mazungumzo, njoo tuzungumze inatoa fursa kwa Waheshimiwa Madiwani kueleza changamoto na vipaumbele kwenye kata zao, kikao hiki kiwe chachu ya mahusiano na mawasiliano baina ya Madiwani na TANESCO,hakikisheni mnawasiliana ili kupata ufumbuzi wa changamoto zinazojitokeza” amesema Samizi.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna inavyotoa fedha nyingi kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo ya umeme.

“Serikali ya awamu ya sita inaupiga mwingi, sisi Serikali na TANESCO tumekubaliana kuwa ifikapo mwezi Februari mwaka 2024 kila Kijiji kipate huduma ya umeme. Hii ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwani ilani imeelekeza wananchi wanapatiwe huduma ya umeme” amesema.

“Ni lazima tutambue kuwa Umeme siyo anasa bali umeme ni huduma ya msingi katika ulimwengu huu wa sasa. Umeme ni Maisha, umeme ni uchumi hivyo ni lazima wananchi wapate huduma ya umeme. Na tunapopeleka huduma za umeme ni vyema pia tuyatambue maeneo yenye huduma za kijamii mfano zahanati na shule” ameongeza Samizi.

Kwa upande wake, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Leo Mwakatobe amesema serikali inaendelea kutekeleza miradi ya umeme katika maeneo mbalimbali mkoani Shinyanga ikiwemo miradi ya REA na Mradi wa mkubwa Umeme Jua wilayani Kishapu huku akiwatoa hofu wananchi kuwa itaendelea kuyafikia maeneo yenye changamoto ili kuhakikisha kila mwananchi ananufaika na huduma ya umeme.

“Tumekutana na Waheshimiwa Madiwani ili tuzungumze. Mhe. Diwani kama una shida usiilaze, piga simu muda wowote tutatoa ufafanuzi kuhusu changamoto yoyote. Naomba madiwani wote muwe na simu zangu (Meneja Tanesco Mkoa) , simu za Afisa Uhusiano na Mainjinia wa wilaya ambao mtawasiliana nao kuhusu mahitaji mbalimbali ili yapate ufumbuzi” amesema Mhandisi Mwakatobe.

"Ni vizuri tukawa na mawasiliano, tuzungumze yanayotukabili ili tuyatatue. Madiwani mtatusaidia kutoa ufafanuzi kwa wananchi. Serikali inatoa fedha kila mwaka kwa ajili ya kusambaza umeme,naomba Waheshimiwa madiwani mfanye kazi kwa ushirikiano na TANESCO ili kutimiza malengo ya serikali ya kuhakikisha kila Kijiji kinafikiwa na huduma ya umeme" ameongeza.

Nao Madiwani walioshiriki kikao hicho licha ya kueleza changamoto na vipaumbele kwenye maeneo yao pia wamempongeza Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga kwa kuandaa kikao hicho ambao kitasaidia kwa kiasi kikubwa kuimarisha mahusiano na mawasiliano baina ya Madiwani na TANESCO ili wananchi wapate huduma ya umeme.

Aidha Madiwani hao wameomba baadhi ya maeneo Mjini Shinyanga ambayo hayana huduma ya umeme hususani yenye sifa za vijiji yaunganishiwe umeme kwa mfumo wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kulipia shilingi 27,000/= kama wanavyopewa wananchi waliopo vijijini kwani wengi wao hawana uwezo wa kumudu gharama kwa mfumo wa gharama zinazotozwa kwa wananchi wa Mjini.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Johari Samizi akizungumza wakati akifungua kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga Jumatano Novemba 15, 2023.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Johari Samizi akizungumza wakati akifungua kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Johari Samizi akizungumza wakati akifungua Kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Johari Samizi akizungumza wakati akifungua Kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Leo Mwakatobe akizungumza kwenye kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Leo Mwakatobe akizungumza kwenye kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Leo Mwakatobe akizungumza kwenye kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Leo Mwakatobe akizungumza kwenye kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Naibu Mstahiki Meya Manispaa ya Shinyanga, Zamda Shaban akizungumza kwenye kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Naibu Mstahiki Meya Manispaa ya Shinyanga, Zamda Shaban akizungumza kwenye kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga.
Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga kikiendelea.
Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Kikao cha TANESCO na madiwani wa Manispaa ya Shinyanga kikiendelea.

No comments:

Powered by Blogger.