LIVE STREAM ADS

Header Ads

Vituo vya Taarifa na Maarifa ubungo vyajadili bajeti yenye mrengo wa kijinsia

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kupitia Vituo vya Taarifa na Maarifa Wilaya ya Ubungo wamekutana kuichambua bajeti ya 2023/2024 yenye mrengo wa Jinsia ambapo wameangalia katika upande wa miundombinu ya Elimu,  Afya, Maji,Kilimo na Miundombinu ya barabara.

Akizungumza na waandishi wa habari Desemba 30,2023 Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kituo Cha Taarifa na Maarifa  kata ya Manzese, Theresia Lehanjara amesema kuwa kwenye maeneo ya elimu wameangalia miundombinu ya shule, kupatikana kwa vyumba vya kujisitiri kwa wasichana, uwiano wa matundu ya vyoo pamoja na uwepo wa vyoo kwa wenye ulemavu.

Aidha wameipongeza halmashauri ya Wilaya hiyo kwani imekuwa ikileta matumaini mazuri hasa kwenye eneo la elimu, wamewekeza fedha za kutosha katika kuimarisha miundombinu ya shule kwenye maeneo mbalimbali.

“Licha yakuwa kuna maeneo ambayo bado kuna changamoto, tunaamini mpaka kufikia mwezi wa sita matarajio mengi yatakuwa yamefikiwa kama watakuwa wamewekeza nguvu kwa wale watendaji” amesema

Amesema kuwa katika Wilaya yao hakuna uwiano sawa wa walimu wakuu wakike na wakiume ambapo imechangia changamoto kubwa ya kutatua mahitaji ya mtoto wa kike anapokuwa shuleni,ambapo wamebainisha pia kuhusiana na miundombinu ya madarasa kubadilishwa kuwa maabara ingawa madarasa hayajitoshelezi.

"Tunaomba basi kama wizara inawaamini wanawake, inapaswa kuwawezesha hawa wanawake wanapochaguliwa kuwa wakuu wa shule, tusisikie habari ya kwamba mwanamke amechaguliwa amekataa kuitumikia ile nafasi, kwanini wanaume wakipata nafasi wanapata uhamisho wao na wenzi wao. Jambo jingine ni madawati na majengo wanataka kuboresha maktaba kwenye mashule yetu tulipokua tukiangalia bajeti tunaomba wasipunguze madarasa kuwa maktaba maana majengo yaliyopo hayajitoshelezi" amesema.

Vilevile amesema kuwa  bado wanakabiliwa na changamoto ya wodi ya wakinamama wajawazito kwa ajili ya kujifungua wanapohitaji huduma hiyo ambapo serikali inatakiwa kushughulikia changamo hiyo kwa haraka.

Kwa upande wake Mwalimu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Lihoya Chamwali amesema kuwa Bajeti yenye mlengo wa kijinsia ni muhimu ili kuhakikisha maendeleo yanamfikia kila mtu ambapo amesema wamebaini kuhusiana na suala la taulo za kike kuwa zimepungua kutoka Milioni mbili hadi kufikia Milioni Moja.

"Tulipewa ufafanuzi kuwa kuna pesa nyingine imetengwa na  hiyo ni kwaajili ya mapato ya halmashauri ya ndani, kuna pesa nyingine ambayo imetengwa kutoka vyanzo vingine hadi kufikia Milioni Kumi" amesema Lihoya.

Naye Kaimu Mwenyekiti wa Kituo Cha Taarifa na Maarifa Kata ya Mabibo, Msafiri Mwajuma ameeleza kuwa bila miundombinu rafiki kwa mwanamke, haitawezekana kumuinua kiuchumi hivyo kunahitajika kutengeneza mazingira wezeshi.

No comments:

Powered by Blogger.