LIVE STREAM ADS

Header Ads

Magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo shinikizo la damu yaongezeka kwa vijana

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Magonjwa yasiyoambukiza ambayo zamani yaliwapata zaidi wazee yametajwa kuongezeka kwa vijana ambapo utafiti umeonyesha ongezeko la uwiano wa vijana wenye shinikizo la damu lililoongezeka kutoka 0.2% hadi 25.1% Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeripoti ongezeko za aina tano za kisukari aina ya kwanza miongoni mwa watoto na vijana kati ya mwaka 2011 na 2021.

Ameyasema hayo Januari 19, 2024 jijini Dar es Salaam Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu katika mkutano wa tano wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili tafiti za afya kwa vijana wa rika balehe na lishe kwa vitendo na sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Amesema kuwa wakati maendeleo makubwa yamepatikana, dhahiri katika kupunguza matokeo duni ya lishe kama vile kudumaa kutoka 34.7% katika 2014 hadi 31.8% mwaka 2018, anemia kati ya wanawake wa umri wa uzazi imepungua kutoka 44.8% katika 2015 hadi 28.8% kwa mwaka 2018 pamoja na kupungua kwa maambukizi mapya ya VVU, hata hivyo baadhi ya maeneo ya vijana kama vile afya ya akili bado yanahitaji juhudi zaidi.

Aidha amesema kuwa tunahitaji ushahidi zaidi wa kisayansi ambao unaweza kuchangia kuimarisha utendaji wa sekta yetu ya afya na ushirikiano ulioonyeshwa hapa kwamba kuhusisha wanasayansi mbalimbali na wataalam wa afya ya umma wa ndani na nje ya Tanzania ambao ni mfano wa kuigwa.

"Nimefurahi kuona Taasisi zetu za Serikali kama Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi ya Jamii Muhimbili, Chuo Kikuu cha Dodoma, Halmashauri mbalimbali za mikoa na Wilaya, Taasisi ya Afya ya Ifakara, Taasisi ya MDH pamoja na ZAPHA+ kutoka Zanzibar zikiwa sehemu ya kazi hii" ameeleza Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesisitiza juu ya umuhimu wa kuendeleza ajenda ya afya miongoni mwa vijana ili kuboresha afya na ustawi wao kwa ujumla, kuinua kizazi cha afya na watu wenye kinga kali, uwezo wa kufikiri kwa umakini na wenye ubora kitaaluma ambayo itachangia maendeleo ya taifa letu.

"Ninatoa wito kwa kila mmoja wetu, watunga sera, watafiti, watoa huduma za afya, wazazi, wanajamii na vijana kuibebaa ajenda hii. Mafanikio haya hayawezi kupatikana bila kushirikiana na washirika wa ndani na wa kimataifa na wafadhili" amesema.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Africa Academy for Public Health (AAPH), Mary Sando amesema kuwa jukumu muhimu katika kuitisha Mtandao wa ARISE unaojumuisha taasisi wanachama 21 kutoka nchi tisa (Botswana, Burkina Faso, Ethiopia, Ghana, Nigeria, Rwanda, Afrika Kusini, Tanzania na Uganda) za Kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo umekuwepo kwa miaka mingi kutokana na ushirikiano wa ndani na kimataifa na umesaidia kupitisha ruzuku,maombi, na usambazaji na tafsiri ya matokeo ya kisayansi yenye athari katika programu zinazoweza kutekelezeka.

Aidha amesema azma yao katika mkutano huo ni kusudi endelevu la kuziba pengo la utafiti kwa kupitia njia shirikishi ya mafunzo kwa lengo la kujenga uwezo na tafsiri ya maarifa.

"AAPH imeendelea kudumisha mashirikiano na vyombo mbalimbali ndani na nje ya nchi kwa kushirikiana na Wizara ya Afya,Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoana Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Taasisi za ndani na nje ya nchi kama vile MUHAS, UDOM na HIGH, pamoja na shirika letu dada la MDH ambapo tunawasaidia katika shughuli za utafiti na kuhakikisha ubora wa data ili kufahamisha ufanyaji maamuzi" amesema Mary Sando.
Na Emmanuel Mbatilo, Dar
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akizungumza katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akizungumza katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati akizungumza katika Mkutano wa tano wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akikabidhiwa tuzo maalumu ya kutambua mchango anaoutoa kwenye sekta ya afya kwa kushirikiana na taasisi zisizo za kiserikali katika Mkutano wa tano wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.


Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Africa Academy for Public Health (AAPH), Mary Sando katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akizungumza jambo na mwakilishi kutoka Chuo Kikuu cha Harvard, Mark Elliott katika Mkutano wa 5 wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Mtendaji wa Taasisi ya Africa Academy for Public Health (AAPH, Mary Sando akizungumza katika mkutano wa tano wa kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Michael Battle akizungumza katika Mkutano wa tano wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Baadhi ya wadau mbalimbali wakiwa katika Mkutano wa tano wa Kisayansi wa “ARISE Network” wenye lengo la kubadili Tafiti za Afya kwa Vijana wa rika balehe na Lishe kwa vitendo na Sera zinazoweza kutekelezwa Kusini mwa Jangwa la Sahara ambao umefanyika Januari 19,2024 kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

No comments:

Powered by Blogger.