LIVE STREAM ADS

Header Ads

Vijana 58 wahitimu mafunzo ya utengenezaji Vihenge

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (wa nne mbele kushoto), viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia) akikagua Vihenge vilivyotengenezwa na Vijana walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo.


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Jumla ya Vijana 58 kutoka mikoa ya Tabora, Mwanza, Geita na Simiyu wamehitimu mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa ‘Tanzania Initiative For Preventing Aflatoxin Contamination – TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo wenye lengo la kuimarisha usalama wa chakula kwa wananchi na kuimarisha afya ya jamii.

Akizungumza Ijumaa Aprili 26,2024 wakati wa kufunga Mafunzo ya kutengeneza Vihenge awamu ya tatu, Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban amesema mafunzo hayo yamehitimishwa rasmi baada ya kutolewa katika awamu tatu yakinufaisha vijana 58.

“Mafunzo ya kutengeneza vihenge yalianza tarehe 26,2024 kwa awamu ya kwanza ambapo washiriki walikuwa 19, ikafuatia awamu ya pili ikiwa na washiriki 23 na leo washiriki 16 wamehitimu. Wamefundishwa masuala ya ujasiriamali, utengenezaji wa vihenge kwa nadharia na vitendo, nadharia ya masoko, usimamizi wa fedha na urasimishaji wa biashara” amesema Taban ambaye ni Afisa Uendelezaji Biashara SIDO Mkoa wa Shinyanga.

“Serikali kupitia mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo imeendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kuimarisha usalama wa chakula kwa wananchi na kuimarisha afya ya jamii. Mradi wa TANIPAC unalenga kuwezesha jamii kutumia njia sahihi na za kisasa za uhifadhi wa nafaka hususani mahindi kutokana na sumukuvu” ameongeza Taban.

Amefafanua kuwa, Serikali imeingia gharama kuhakikisha kuwa vijana wanapatiwa ujuzi wa kutengeneza vifaa vya kisasa na vinavyodumu kwa muda mrefu (vihenge) ili kutimiza adhima ya kupunguza sumukuvu.

Taban amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuhakikisha wanayatumia kwa vitendo kuhakikisha kuwa lengo la mafunzo linatimia ambapo pia yatawezesha kuongeza kipato cha mmoja mmoja, kaya na taifa kwa ujumla.

“Mafunzo haya yametolewa kwa vijana wachache lakini wengi wangependa kupata mafunzo haya,hivyo nitumie nafasi hii kuwaomba mkawe waalimu wa kufundisha vijana wenzenu kwenye maeneo yenu ya kazi ili kwa pamoja tuweze kupambana kwa vitendo kupunguza kama siyo kuondoa kabisa sumukuvu” amesema Taban.

Akisoma risala kwa niaba ya Washiriki wenzake wa mafunzo, Wanjala Daudi amesema mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha utendaji kazi na kuzalisha bidhaa za vihenge (Silos) na nyinginezo kwa tija ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

“Tunaushukuru uongozi wa SIDO na Wizara ya Kilimo kwa kutoa fursa ya mafunzo haya. Hakika mafunzo haya yametujengea uwezo wa kujiamini na kuamsha ari ndani yetu ya kujiajiri na kuachana na kasumba ya kusubiri ajira” amesema Daudi.

“Pamoja na ari na motisha ya kujiajiri iliyojengeka ndani yetu, tunakabiliwa na changamoto ya mitaji kwa ajili ya kununua vifaa/vitendea kazi vya kuanzisha shughuli mbalimbali kutokana na fani tulizojifunza” ameongeza Daudi.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa vijana wakati akikagua Vihenge vilivyotengenezwa na Vijana walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa ‘Tanzania Initiative For Preventing Aflatoxin Contamination – TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kushoto) akikagua Vihenge vilivyotengenezwa na Vijana walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (wa nne mbele kushoto) , viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo wenye lengo la kuimarisha usalama wa chakula kwa wananchi na kuimarisha afya ya jamii.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Mratibu wa Mafunzo ya Kutengeneza Vihenge Mkoa wa Shinyanga, Misuka Makwaya ambaye ni Mhasibu wa SIDO Mkoa wa Shinyanga akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Mratibu wa Mafunzo ya Kutengeneza Vihenge Mkoa wa Shinyanga, Misuka Makwaya ambaye ni Mhasibu wa SIDO Mkoa wa Shinyanga akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Wanjala Daudi akisoma risala ya washiriki wa mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Afisa Mipango SIDO Shinyanga, Frank Nguyu akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Mwenyekiti wa Mafunzo, Charles Kulwa akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Mratibu wa Mafunzo SIDO Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Manyama Lububi akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Jumanne Joseph Taban, viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga, Joseph Taban, viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo.

No comments:

Powered by Blogger.