LIVE STREAM ADS

Header Ads

Ruhoro Achukua Fomu Kuwania Ubunge Ngara

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com

    



Mbunge wa jimbo la Ngara Mhe. Ndaisaba George Ruhoro amechukua fomu ya maombi ya kugombea tena nafasi ya ubunge kwa kipindi kingine cha 2025/30 kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Fomu hiyo ameichukua leo Juni 30 2025 katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi CCM Ngara Mkoani Kagera. 

 Hata hivyo vyombo vya habari vilivyokuwepo katika eneo la tukio walipotaka mahojiano hakuwa tayari kuzungumzia chochote zaidi alisema wakati ukifika atazungumza.

Ikumbukwe kuwa Mheshimiwa Ruhoro ni miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa  kwa wananchi wa jimbo lake kwani wananchi hao wamekuwa wakimchangia fedha kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea tena katika kipindi kingine 2025-2030.

No comments:

Powered by Blogger.