LIVE STREAM ADS

Header Ads

UTEKELEZAJI MRADI WA HEET WwafikiaAFIKIA ASILIMIA 7474.3, SERIKALI YAPONGEZWA

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com

Mratibu wa Mradi, kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Kenneth Hosea, akizungumza wakati wa kumkaribisha Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa kikao cha Mradi wa HEET

Na Mwandishi Wetumpka. 

UTEKELEZAJI wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) umefikia asilimia 74.3 tangu uanze kutekelezwa mwaka 2022, hatua iliyotajwa kuwa mafanikio makubwa.

Hayo yameelezwa leo Septemba 15,2025 , katika ukumbi wa Maktaba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Mratibu wa Mradi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Kenneth Hosea, wakati akimkaribisha Mgeni rasmi kufungua kikao cha siku tano cha tathmini ya Mradi, kikihusisha wadau wote muhimu wanaotekeleza Mradi huo.

Dkt. Hosea amesema, juhudi hizi kubwa ni matokeo ya kazi nzuri iliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwamba Wizara inaendelea kutoa hamasa kwa Taasisi za Elimu ambazo zinatekeleza mradi huu kuendelea kuongeza kasi ili kuhakikisha malengo yanafikiwa katika kipindi kilichopangwa.

Akifungua kikao kazi hicho, mgeni rasmi, Prof. Nelson Boniface, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akimwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo amesema inatia moyo kuona mafanikio makubwa ya Mradi kitaifa na kuwataka washiriki katika kupokea mawasilisho kuwa makini kujifunza na kutumia fursa hiyo kujifunza kutoka kwa wale waliofanikiwa ili kwa pamoja kufikia malengo makubwa kama Taifa.

“Hii ni fursa kwa Taasisi ambazo bado ziko nyuma kwenye utekelezaji, tuitumie kwa kujifunza wenzetu walikopita wakafanikiwa ili tuongeze juhudi za tufikia malengo yaliyokusudiwa” Alisisitiza.

Katika Mkutano huo, Mratibu msaidizi wa Mradi Chuo Kikuu cha Dodoma, Dkt. Happiness Nnko, amewasilisha taarifa ya maendeleo ya Mradi kwa kueleza baadhi ya Miradi imekamilika kwa asiliamia 100, wakati miradi ya ujenzi ikiendelea kutekelezwa ukiwemo ujenzi wa Maabara ya Sayansi katika Ndaki ya Sayansi Asilia na Hisabati, ambapo ujenzi wake umefika asiliamia 55.3, Ujenzi wa vyumba vya Madarasa Ndaki ya Sayansi za Ardhi ya Uhandisi umefikia asilimia 61, wakati ujenzi wa Kampasi Mpya, Njombe ulioanza mwezi Juni 2025, umefikia asilimia 10.3.

Amesema,kuwa Menejimenti ya Chuo inaendelea kufuatilia kwa karibu ujenzi unaoendelea ikiwemo vikao vya mara kwa mara na wakandarasi, ili kuhakikisha ujenzi unakamilika kabla Mradi kwisha, Juni 2026. Kwa upande wa mitaala mipya ya elimu, Dkt. Nnko amesema Chuo kimefanikiwa kubuni na kufanya mapitio ya programu 39, na mchakato wa kuzianzisha uko kwenye hatua mbalimbali za mapitio na kupata ithibati.

“Mbali na mapitio ya programu, pia Chuo kimepeleka Wakufunzi 18 masomoni kwa ngazi mbalimbali za elimu (Masters na PhD), kati yao wanaume wakiwa 13 na wanawake watano(5). Baadhi wanasoma hapa Tanzania na wengine wako nje ya nchi, Ghana, Uganda, Africa Kusini, Uingereza, Japan na Zambia.

Aidha, Chuo kinaendelea na ununuzi wa vifaa na samani vya majengo, ambapo hadi kufika Septemba 15, 2025 tayari manunuzi 23 yameanzishwa, kati ya hayo 11 wazabuni wameshapatikana, huku taratibu za manununi kwa maeneo mengine zikiendelea.

Mkutano huu umekutanisha Waratibu wa Mradi kutoka kwenye Taasisi zote za Elimu ya Juu nchini zinazotekeleza Mradi wa HEET, waratibu Wasaidizi, Wataalamu wa Maeneo mbalimbali ya Mradi ikiwemo Ufuatiliaji na Udhibiti, Mazingira, Tehama, Mahusiano na Viwanda na Mawasiliano.


,Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Nelson Boniface,akifungua Kikao Kazi cha Waratibu na Wasimamizi wa Mradi wa HEET kilichoanza leo Dar es Salaam.


Mratibu wa Mradi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Kenneth Hosea, akizungumza wakati wa kumkaribisha Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa kikao cha Mradi wa HEET

 

Mratibu Msadizi wa Mradi wa HEET toka Chuo Kikuu cha Dodoma, Dkt. Happiness Nnko, akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya Mradi kwa UDOM wakati wa Kikao cha Wadau.
Mratibu wa Mradi wa HEET toka Chuo Kikuu cha Dodoma akisikiliza kwa makini wasilisho wakati wa kikao cha wadau kinachoendekea katika ukumbi wa Maktaba, UDSM
  Baadhi ya washiriki wa kikao kazi wakifuatilia kwa makini kikao kuhusu maendeleo ya Mradi wa HEET

No comments:

Powered by Blogger.