ALICHOKISEMA WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII WAKATI AKIWAKABIDHI TUZO WASHINDI WA HABARI ZA TANAPA MWAKA 2013/14.
![]() |
Mh.Nyalandu |
Mh.Nyalandu aliyasema hayo jumanne ya wiki hii May 27 Mkoani Mwanza,
katika hafla ya kuwakabidhi tuzo washindi wa Tuzo za Shirika la Hifadhi za
Taifa nchini TANAPA mwaka 2013/14 zinazohusiana na Uandishi wa Makala za Utalii
kupitia Radio, Luninga na Magazeti.
Alisema Waandishi wanapozishika kalamu zao wajue wanaifanya kazi ya
Watanzania, hivyo waifanye kazi hiyo kwa uhuru mkubwa, huku akibainisha kwamba
habari watakazoziandika juu ya kupambana na Ujangili zitasaidia kuinua hali ya
Utalii hapa nchini, ikiwa ni pamoja na kuwaandika wale wote wanaojihusisha na
biashara hiyo haramu ya ujangili.
Zaidi aliwasisitia wanahabari kwamba wanapaswa Kuifanya kazi ya
kuielimisha jamii kupitia habari zinazohusiana na vivutio pamoja na hifadhi
mbalimbali za Utalii hapa nchini ili kuwafanya wananchi wa kawaida kupenda
raslimali za nchi yao.
Aidha alibainisha kwamba katika mwaka wa 2014/15 ameandaa mpango
maalumu wa Kuhuiisha Mtazamo wa Tanzania katikaki ya Mataifa na kuifanya
Tanzania kuondokana na hali ya kulalamika bali kuifanya dunia ishangazwe na
Tanzania hali ambayo pia itabadilisha idadi ya watalii nchini hadi kufikia
watalii Milioni Mbili mwaka 2015/17 kutoka watalii Milioni 1.1 kwa mwaka
2012/13.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi
za Taifa nchini TANAPA, Alan Kijazi aliwataka waandishi wa habari kuwa na Umoja
katika kufanya kazi zinazohusiana na utalii kwa kuwa TANAPA iko tayari
kuwasaidia waandishi wa habari kupitia umoja wao.
Alisema kwa sasa TANAPA inashindwa kuwasaidia waandishi wa habari
wanaoandika habari za utalii kupitia vyama vyao, na hivyo kuwasihi waandishi wa
habari za Utalii kuwa na Chama kimoja ambacho TANAPA inaweza kushirikiana nacho
katika uandishi wa habari za Uhifadhi na Utalii, huku akiweka wazi kwamba
TANAPA iko tayari kusimamia mafunzo ya Uandishi wa habari za Uhifadhi na Utalii
kwa wanahabari.
KUHUSU
TUZO ZA TANAPA
Nazo Tuzo za TANAPA mwaka 2013/14 ziligawanyika katika Makundi mawili ambapo kulikuwa na kundi la kwanza ambalo lilikuwa linahusiana na Makala zinazohusiana na Utalii wa Ndani, pamoja na kundi la pili ambalo lilikuwa linahusu Masuala ya Uhifadhi. Ambapo katika Tuzo hizo kulikuwa na washindi watatu kutoka katika kila mgawanyo wa vyombo vya habari ambavyo ni Radio, Luninga na Magazeti ama Mitandao ya Kijamii (Blogs).
Katika Tuzo hizo Mshindi wa Kwanza alijinyakulia Hundi ya Shilingi
Milioni mbili, cheti, ngao pamoja na Safari ya Kimafunzo katika mojawapo ya
nchi za Kusini mwa Bara la Afrika, na Mshindi wa Pili akijipatia Hundi ya
Shilingi Milioni moja na nusu, cheti pamoja na safari ya kimafunzo katika
hifadhi mbili za Kitaifa hapa nchini, huku mshindi wa tatu akijipatia Hundi ya
Shilingi Milioni moja pamoja na cheti. Zawadi hizo zikiwa ni linganifu kwa
washindi wa Radio, Luninga na Magazeti.
Washindi
wa Tuzo za TANAPA 2013/14 kundi la Utalii wa ndani
Washindi
wa Tuzo za TANAPA 2013/14 kundi la Masuala ya Uhifadhi
Upande wa Magazeti mshindi wa kwanza na wa Pili hawakuweza kupatikana
kutokana na kutofikia vigezo vya majaji, Mshindi wa Tatu alikuwa ni Salome
Kitomali kutoka Nipashe. Upande wa Radio Mshindi wa Kwanza pia hakuweza
kupatikana, Mshindi wa Pili alikuwa ni David Rwenyagila huku mshindi wa Tatu
pia akishindwa kupatikana. Na upande wa Luninga Mshindi wa Kwanza alikuwa ni
Vedasto Msungu kutoka ITV, Mshindi Wa Pili Raymond Nyamwihula wa Star TV ambapo
mshindi wa Tatu upande wa Luninga pia hakuweza kupatikana.
Kwa mjibu wa Mwenyekiti wa Jopo la Majaji wa Tuzo hizo za TANAPA
2013/14 Dk.Ayub Rioba ambae ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni
Kwamba nafasi ambazo washindi hawakupatikana zilitokana na Jopo la majaji
kutoridhika na makala zilizowasilishwa kulingana na vigezo vilivyokuwa
vimewekwa. Ambapo miongoni mwa vigezo hivyo ni pamoja na Makala kutokuwa na
udhamni wa aina yoyote kutoka TANAPA, kuwa na uthibitisho kutoka kwa Mhariri wa
chombo husika, na iwe haijawahi kutumwa katika tuzo zilizopita sanjari na kuwa
imetumika katika kipindi cha kati ya mwezi wa Kwanza hadi mwezi wa 12 mwaka
uliopita.
No comments: