LIVE STREAM ADS

Header Ads

Director Tyson wa Bongo Movie Afariki dunia......Aacha mwendelezo wa Simanzi kwa Wapenzi wa Bongo Movie hapa nchini.

Gari alilopatanalo ajali Director Tyson
Mwongoza wa Bongo Movie George Tyson ambae pia ni Mme wa Staa wa Bongo Movie Yvonney Cherry maarufu kama Monalisa, amefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Mkoani Dodoma kwenda Jijini Dar es Salaam kuoata ajali Mkoani Morogoro. 
 
Dj Choka ambae kwa sehemu kubwa alikua kwenye safari moja ya Dodoma na Marehemu George Tyson, ameandika kwamba Marehemu alikuwa yupo kijiji cha Chilonwa Chamwino kwenye utoaji wa madawati katika shule ya msingi Chaula iliyopo Dodoma.
 
"Baada ya kumaliza shughuli hii huku akiwa kama producer wa The Mboni Show mauti yalimkuta majira ya saa 12 jioni ikiwa ni saa 4 tu toka tuanze safari ya kurudi Dar es Salaam maeneo fulani hivi kama unataka kukaribia GAIRO mjini" Ilieleza taarifa ya Dj Choka na kuongeza...
"Kwenye gari walikuwa watu 8 ila yeye pekee ndio aliyepoteza maisha ila wengine wamepata majeraha mwilini akiwemo dereva wa gari hilo ambapo kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa hapa Morogoro katika hospital ya mkoa Morogoro baadae asubuhi safari ya kurudi Dar es Salaam itaanza".
Ajali hiyo inaelezwa kuwa ajali mbali ambapo baadhi ya majeruhi wamelazwa katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya matibabu.
Gari alilopatanalo ajali Director Tyson
 
Tyson akiwa na Mboni Masimba wa The Mboni Show kabla ya umauti wake Mkoani Dodoma.
 MTANZANIA MEDIA TUNATOA POLE KWA NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI WALIOGUSWA NA MSIBA HUU. R.I.P TYSON ......Info. Kwa ushirikiano na Dj Choka.

No comments:

Powered by Blogger.