UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KUFANYIKA KESHO, JIJI LA MWANZA KUWA MWENYEJI WA MAADHIMISHO HAYO KITAIFA. SOMA ALICHOKISEMA MTUMISHI WA MUNGU KUHUSIANA NA MAADHIMISHO HAYO.
![]() |
Konisaga (Mtumishi wa Mungu) |
Katika
Taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo iliyosomwa jana na
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga (Mtumishi wa Mungu) ambae anakaimu
Ofisi yake, ilieleza kwamba Maadhimisho hayo yanatarajiwa kufunguliwa kesho
katika Uwanja wa Furahisha Mkoani Mwanza na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Mazingira Dkt.Binilith Mahenge.
Taarifa hiyo
ilibainisha kwamba katika juma la Maadhimisho hayo ya Siku ya Mazingira,
shughuli mbalimbali zitafanyika ikiwa ni pamoja na kufanya usafi katika maeneo
yote, kuhamasisha wananchi kuhusiana na utunzaji wa mazingira kwa njia ya
makongamano.
Shughuli
nyinge ni kupanda miti, kuzoa takataka, maonyesho ya utunzaji wa mazingira,
kuondoa magugu maji katika ziwa Victoria, ufugaji wa nyuki pamoja na kufanya
ziara katika maeneo yanayojishughulisha na utunzaji wa mazingira ikiwemo
viwanda.
Mgeni Rasmi
katika kilele cha maadhimisho hayo kitakachofanyika June Tano Mwaka huu,
anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal ambae anatarajiwa kukabidhi
vyeti kwa wadau mbalimbali wa mazingira, zawadi na tuzo ya Rais ya Utunzaji na
Uhifadhi wa Mazingira pamoja na zawadi nyinginezo kwa washindi wa Uhifadhi wa
Mazingira.
“Natambua
kwamba ninyi ni wadau wakubwa sana wa Mazingira hasa katika jukumu lenu la
kuelimisha umma, juu ya umuhimu wa kutunza mazingira, kwa nafasi ya pekee
niwaombe muweze kuipeleka taarifa hii kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza na maeneo
ya jirani ili waweze kujitokeza kwa wingi katika Viwanja vya Furahisha kwa muda
wote ambao elimu kuhusu utunzaji wa mazingira itakuwa ikitolewa na wadau
mbalimbali” Alisema Konisaga wakati akizungumza na wanahabari.
Aidha
Konisaga alihitimisha kwa kwa kutoa rai kwa wananchi wa Mwanza kujitokeza kwa
wingi na kushirikiana na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi
watakaofika Jijini Mwanza kwa ajili ya Maadhimisho hayo kwa kuonyesha ukarimu
wa hali ya juu kama ilivyo ada ya wanamwanza, sanjari na kuwahimiza kuzingatia
usafi katika maeneo yao ili kuwezesha Jiji la Mwanza kuendelea kuwa Jiji Safi katika
Mashindano ya Majiji hapa nchini.
![]() |
Konisaga Kushoto, Kulia ni Madete |
![]() |
Angelina Madete |
Tayari Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Angelina Madete yuko Mkoani Mwanza kwa
ajili ya kukamilisha maandalizi ya Maadhimisho hayo ya Siku ya Mazingira duniani,
ambapo katika Maelezo yake alieleza kwamba siku hii inakumbusha juu ya umhimu
wa kutunza mazingira katika maisha kwa kuzingatia uzalishajimali ambao
hauathiri uhifadhi na utunzaji wa Mazingira.
Kauli mbiu
ya maadhimisho hayo Kimataifa ni “Chukua Hatua Kukabiliana na Mabadiliko”
ambapo Kitaifa ni “Tunza Mazingira ili Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi”
zote zikiwa mahsusi kwa ajili ya kuhimiza juu ya umuhimu wa Uhifadhi wa
Mazingira.
No comments: