LIVE STREAM ADS

Header Ads

FASTJET YAFUNGUA OFISI MPYA AIRPOT MKOANI MWANZA……ATAKAE NUNUA TIKETI KATIKA OFISI HIYO SIKU YA KESHO, KUPATA OFA BABU KUBWA.


Wafanyakazi wa FastJet
Kampuni ya Usafirishaji wa Safari za Anga FastJet, Leo imezindua Ofisi yake Mpya ya Mauzo ya Tiketi eneo la Airpot Mkoani Mwanza, kwa lengo la Kuwarahisishia wateja wake urahisi wa kununua tiketi, jambo litakalosaidia pia kuondokana na Msongamano wa wateja wakati wa Manunuzi ya Tiketi.
 
Akizungumza katika Ufunguzi wa Ofisi hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo, Kamimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela James Chuwa aliipongeza Kampuni ya FastJet kwa kurahisisha usafiri wa anga hapa nchini kupitia huduma zake za Usafiri wa anga.

Aidha Chuwa alieleza kwamba, pamoja na huduma bora zinazotolewa na Kampuni hiyo bado kuna baadhi ya changamoto ambazo wateja wa FastJet wanazilalamikia hivyo ni vyema zikatafutiwa ufumbuzi.

“…Lakini pia niseme tumekuwa tukikumbana na changamoto mbalimbali ofisini, wananchi wetu wakitulalamikia… wamekuwa wanasema wamekuwa wanatozwa gharama kubwa sana kupitia mizigo yao, hilo kwenu lipokeeni kama changamoto na muangalie namna ya kurahisisha bei ya mizigo…” Alisema Chuwa.

Kwa upande wake Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza Easter Madale, aliongeza kuwa suala la gharama za tiketi za FastJet lingeangaliwa upya ili kiwango cha gharama cha tiketi za bei ya chini zisiwe na tofauti kubwa na tiketi za gharama ya juu ili watu wote waweze kunufaika na huduma za Kampuni hiyo ya FastJet.


Pia aliusihi uongozi wa FastJet kuongeza huduma zaidi katika Ofisi hiyo na kutoa pia huduma nyinginezo kama vile huduma kwa wateja, badala ya kutoa huduma kwa ajili ya Mauzo pekee ili kuwarahisishia wateja wake upatikanaji wa huduma karibu zaidi.

Nae Meneja Masoko wa FastJet Jean Uku aliahidi kuwa Kampuni yake italishughulikia suala la gharama za usafirisha wa mizigo ya wateja wa FastJet, huku akibainisha kwamba Mteja atakae nunua tiketi ya Safari siku ya kesho atapata ofa ya kusafirisha mizigo yake bure kabisa.

“Nimesikia hiyo na tutaangalia juu ya bei ya mizigo, lakini kwa kuanza kesho tutakuwa na ofa kwa mteja atakae nunua tiketi FastJet katika ofisi yetu mpya, lakini pengine in future (siku zijazo) tutapunguza bei ya kusafirisha mizigo…”.Alibainisha Uku.

No comments:

Powered by Blogger.