LIVE STREAM ADS

Header Ads

HOMA YA DENGUE YAGUNDULIKA KUWEPO JIJINI MWANZA.MTUMISHI WA MUNGU AWATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHARI IKIWA NI PAMOJA NA KUWEKA MAZINGIRA KATIKA HALI YA USAFI.


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dk.Valentino Bangi kulia, na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga (Mtumishi wa Mungu) kushoto wakati wakitoa taarifa ya Kuwepo kwa mgonjwa wa Dengue Mkoani Mwanza katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

 Mgonjwa mmoja amelazwa katika Hospital ya Mkoa wa Mwanza Sekour Tour kwa ajili ya Matibabu zaidi, baada ya kuthibitika kuwa na Maambukizi ya Ugonjwa wa Dengue unaoenezwa na Mbu aina ya Aedes.

Akitoa Taarifa ya Kuwepo kwa Mgonjwa huyo hii leo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga aliwataka wananchi Mkoani Mwanza kuzingatia usafi wa Mazingira sanjari na kuangamiza Mazalia yote mbu katika mitaa yao ili kujikinga na ugonjwa huo.

Aidha alibainisha kuwa Ugonjwa huo huwapata watu wa rika zote japo watoto wenye umri chini ya Miaka Mitano na akina mama wajawazito wana nafasi kubwa ya kuathirika zaidi na ugonjwa huo wa Dengue.

Taarifa hiyo ya Konisaga ilieleza kuwa asilimia 90 ya wagonjwa walioambukizwa ugonjwa huu huonyesha dalili za awali kuanzia siku tatu hadi 14 baada ya kuumwa na mbu aina ya Aedes mwenye maambukizi ya virusi vya vinavyosababisha ugonjwa Dengue.

Mwanahabari Akiuliza Swali juu ya Ugonjwa huo wa Dengue wakati Taarifa ya ugonjwa huo ikitolewa kwa wanahabari.
Wanahabari wakifuatilia taarifa ya Ugonjwa wa Dengue wakati ikitolewa kwao Mkoani Mwanza.
Miongoni mwa dalili za ugonjwa wa Dengue ni pamoja na Homa kali ya ghafla, kuumwa kichwa hususani sehemu za machoni, maumivu makali ya misuli pamoja na viuongo vya mwili, kuvimba tezi, kupatwa na harara sanjari na kichefuchefu au kutapik

Asilimia 10 ya wagonjwa wa Dengue hupatwa na dalili kali kama kutokwa na damu kwenye sehemu za uwazi za mwili kama vile mdomoni, masikioni pamoja na sehemu za siri kama vile sehemu za haja kubwa na ndogo.

Njia mbalimbali zinashauriwa kufuatwa ili kujikinga na Homa ya Dengue, njia hizo ni pamoja na kuzingatia usafi wa mazingira ikiwa ni pamoja na Kuangamiza mazalia ya mbu kutumia vyandarua sanjari na kutumia dawa za kuzuia mbu.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Kulia Baraka Konisaga (Mtumishi wa Mungu), na Mganga wa Mfawidhi Sekour Toure Dk.Onesmo Rwakyendera Kushoto.
 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dk.Valentino Bangi alibainisha kuwa mgonjwa huyo alifika Hospital ya Mkoa Mwanza Sekour Toour jumanne May 20 mwaka huu, na kupewa matibabu bila mafanikio, ambapo jana aliporudi hospitalini alipigwa kipimo cha Dengue na kuthibitika kuwa na ugonjwa huo.

“Tarehe 17 mwezi huu mgonjwa huyu ambae ni mstaafu mzee wa makamo mwenye umri wa miakla 62 alienda Dar es salaama katika Hospital Mhimbili-MOI kwa ajili ya matibabu ya Mifupa na aliporudi ndo alianza kuhisi kuumwa hivyo inaaminika kuwa huko ndiko alikotoka na maambukizi ya Ugonjwa huo”. Alisema Dk.Bangi huku akisisitiza zaidi wananchi kuzingatia usafi wa mazingira ili kuangamiza mazalia ya mbu wanaoambukiza ugonjwa huo.

Katika hatua nyingine Dk.Bangi alisema kuwa ni jukumu la kila mmoja kujikinga na kujilinda na maambukizi ya Ugonjwa wa Dengue, ambapo alibainisha kuwa watalaamu wa Afya Mkoani Mwanza wamejiandaa kikamilifu kwa ajili ya kupambana na ugonjwa huo, ambapo mgonjwa hupewa matibabu kulingana na dalili alizonazo kwa kuwa ugonjwa huo hauna chanjo wala tiba.

“Katika Mkoa wa Mwanza tumepokea vipimo takribani 50 vya kupima ugonjwa huo, ambapo tayari kipimo kimoja kimwekwisha tumika hivyo tumebaki na vipimo 49 ambapo baadhi tumevigawa katika Wilaya za Ukerewe, Kwimba na Sengerema ambapo ambapo hapa Mkoani Tumebaki na vipimo 20 ambapo Wizara inatarajia kuleta vipimo vingine katika Bohari ya dawa Kanda ya Ziwa MSD kulingana na Mahitaji kwa kuwa bado hakuna kasi ya Maambukizi ya Ugonjwa huu”. Alieleza Dk.Bangi.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dk.Valentino Bangi.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure Dk.Onesmo Rwakyendera ambae hakutaka kumtaja mgonywa huyo jina, alibainisha kuwa hatua mbalimbali zinachukuliwa ili kuhakikisha kuwa kila mgonjwa hospitalini hapo analala ndani ya chandarua sanjari na kupata dawa kwa ajili ya kunyunyizia ili kuua mazalia ya mbu hospitalini hapo sanjari na maeneo mengine ya Mkoa wa Mwanza ikiwa ni pamoja na eneo la Kilimahewa ambapo mgonjwa huyo ametokea.

Kuanzia mwezi march mwaka Ugonjwa wa Homa ya Dengue ulianza kugundulika Mkoani Dar es salaam ambapo takribani watu watatu wapepoteza maisha huku wengine zaidi ya 400 wakiwa wameambukizwa ugonjwa, ambapo sasa ugonjwa huo umeanza kueneo katika Maeneo mbalimbali hapa nchini kutokana na muingiliano wa watu.

No comments:

Powered by Blogger.