JIJI LA MWANZA KUTETEA UBINGWA WAKE KWA MARA YA TISA MFULULIZO?
![]() |
Mzunguko wa Samaki Jijini Mwanza |
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Halifa
Hida amebainisha kwamba, Halimashauri ya Jiji la Mwanza inatarajia kuwa
mwenyeji wa Maadhimisho ya Siku ya Usafi na Mazingira Kitaifa, yanayotarajiwa
kuadhimishwa June Tano Mwaka huu.
Akitoa
Taarifa hiyo Wiki hii mbele ya Baraza la Halimashauri ya Jiji la Mwanza wiki iliyopita, Hida
ameeleza kuwa Maandalizi ya Siku hiyo yamekwisha anza, ambapo amewataka
viongozi mbalimbali wa Serikali za Mitaa kuhakikisha Mitaa yote ya Halimashauri
ya Jiji inakuwa katika hali ya Usafi.
Ameongeza
kuwa kwa mara ya Tisa Mwaka huu, Halimashauri ya Jiji la Mwanza inafanya kila
juhudi ili kuhakikisha kwamba inatetembea Ubingwa wake wa kuwa Jiji Safi hapa
nchini, Ubingwa ambao Halimashauri hiyo imekuwa ikiushikilia tangu kuanzishwa
kwa mashindano ya Majiji Safi hapa nchini Mwaka 2006.
Aidha
amewataka wananchi kuhakikisha kuwa wanaweka Mitaa yao katika hali ya Usafi
katika kipindi hiki cha kuelekea katika Maadhimisho hayo, kwa kuwa Jiji la
Mwanza litapokea wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi ambao
watazunguka katika Mitaa mbalimbali ya Jiji kujionea hali ya Usafi wa Mazingira
na Mitaa ya Jiji la Mwanza.
JE JIJI LA MWANZA LINASTAHILI KUTETEA
NAFASI YAKE YA JIJI SAFI HAPA NCHINI MWAKA HUU KWA MARA YA TISA MFULULIZO? JE
SERA YA KUFANYA USAFI KILA JUMAMOSI YA MWANZO WA MWEZI JIJINI MWANZA IMEZAA
MATUNDA? PIA KWA NINI MAENEO MENGI HAPA NCHINI YAKIWA YANAPOKEA WAGENI NDIO
MKAZO WA USAFI UNAHIMIZWA?
No comments: