NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII AZINDUA MPANGO WA NYOTA YA KIJANI MKOANI MWANZA.
![]() |
Picha haihusiana na Uzinduzi |
Dkt.Kebwe alitoa kauli hiyo hii leo Mkoani Mwanza katika Uwanja wa Nyamagana wakati akizindua Mpango wa Nyota ya Kijani katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, Mpango ambao umelenga kuhamasisha wananchi kutumia huduma za Uzazi wa Mpango sanjari na kusogeza karibu huduma hizo kwa wananchi hususani walioko vijijini.
Alibainisha
kwamba matumizi ya Uzazi wa Mpango hapa nchini yako katika kiwango cha chini
ukilinganisha na nchi nyingine duniani, ambapo Kitaifa Matumizi ya Uzazi wa
Mpango yako chini ya asilimia 27 ikilinganishwa na nchi zilizoendelea ambazo zimefikia
kiwango cha zaidi ya asilimia 70.
Akitoa
taarifa ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii juu ya tathimini ya Kiwango cha
Utumiaji wa Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto ambayo inajumuisha huduma ya Uzazi
wa Mpango hapa nchini, Helem Semu ambae ni Kaimu Mkurugenzi Kitengo cha elimu
ya Afya kwa Umma, amebainisha kuwa kiwango cha utumiaji wa Uzazi wa Mpango
katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi kiko chini ukulinganisha na
Mikoa ya Kasikazini.
“Katika Mkoa
wa Mwanza ambao uko Kanda ya Ziwa kiwango cha utumiaji wa Mpango wa Uzazi kiko
chini ya asilimia 12, ukilinganisha na kiwango cha asilimia 50 katika Mkoa wa
Kilimanjaro ulioko Kanda ya Kasikazini”, huku akibainisha kuwa “Wizara inafanya
jitihada ili kuongeza kiwango cha utumiaji wa uzazi wa Mpango katika Mikoa ya
Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi”.Akisema Semu.
Nao baadhi
watumiaji wa Huduma ya Uzazi wa Mpango waliwahimiza wanajamii wengine ambao
hawajajiunga na mpango wa Uzazi wa Mpango kuchukua maamuzi ya kujiunga kwa kuwa
njia za uzazi wa mpango hazina madhara yoyote mbali na kuwa na faida mbalimbali
ikiwemo kupanga familia bora.
Nae Mganga
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt.Valetino Bangi aliwahimiza wananchi kutumia huduma
za uzazi wa mpango, ambapo wataweza kunufaika na faida mbalimbali zitokanazo na
mpango huo ambazo ni pamoja na kupunguza vifo vya watoto sanjari na akina mama
kutokana na ujauzito na uzazi.
Awali
akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mh.Baraka
Konisaga alisisitiza juu ya upatikanaji wa huduma bora za Uzazi wa Mpango kwa
kuwa uzazi wa Mpango unaweza kusaidia kupunguza vifo vya uzazi hadi kufikia
asilimia 44.
No comments: