UZINDUZI WA NYOTA YA KIJANI KWA MIKOA YA KANDA YA ZIWA KUFANYIKA MKOANI MWANZA, NAIBU WAZIRI WA AFYA KUWA MGENI RASMI.
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa Kushirikiana na Wadau wa Afya ya Uzazi inazindua upya Kampeni ya Nyota ya Kijani katika Mikoa Mitano ya Kanda ya Ziwa, ambapo uzinduzi huo unatarajia kufanyika kesho jumanne May 20, 2014 katika Uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.
Akitoa
taarifa ya Uzinduzi huo hii leo kwa Niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa
Wilaya ya Nyamagana Mh.Baraka Konisaga alibainisha kwamba, Uzinduzi huo ni
sehemu ya Mkakati wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ikishirikiana na Asasi
zinazotoa huduma za Uzazi na Mtoto kutoka ndani na nje ya nchi.
Alisema
lengo la Mpango huo wa Nyota ya Kijani ni Kuongeza Kiwango cha Upatikanaji na
Matumizi ya Huduma ya Uzazi wa Mpango katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo
takwimu zinaonyesha kuwa kiwango cha Utumiaji wa Uzazi wa Mpango katika Mikoa
ya Kanda ya Ziwa iko katika kiwango cha chini.
Mikoa inayo
inayohusika na Uzinduzi huo ni Mwanza, Mara, Shinyanga, Simiyu, na Geita ambayo
wastani wakw wa matumizi ya njia za kisasa za Uzazi wa Mpango ni chini ya
asilimia 13 ikilinganishwa na wastani wa Kitaifa wa Asilimia 27.
Kwa mantiki
hiyo Konisaga alibainisha kwamba kampeni hiyo ya Nyota ya Kijani ni kampeni
maalumu ambayo imelenga kuhamasisha wananchi kutumia huduma za uzazi wa mpango
sanjari na kusogeza huduma za uzazi wa mpango kwa wananchi hususani walio
vijijini.
“Uzinduzi wa
Nyota ya Kijani Kitaifa ulifanyika Oktoba 11 mwaka jana na Makamu wa Rais
Dkt.Mohamed Gharib Bilal katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam,
alipotangaza nia ya Serikali ya Kuimarisha huduma za uzazi wa Mpango ili
kufikia ahadi ya Mh.Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ya kufikia kiwango cha matumizi ya huduma za uzazi wa mpango cha
asilimia 60 ifikapo mwaka 2015”.Alisema Konisaga.
Kufuatia mwamko
wa wananchi kutumia uzazi wa Mpango kuwa chini katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa,
Mganga Mkuu wa Mwanza Dkt.Valentino
Bangi alibainisha kuwa ni kutokana na wananchi wake kuwa na imani tofauti
tofauti ikiwemo wazazi kuamini kwamba kuzaa watoto wengi katika familia
kunaleta manufaa mbalimbali yakiwemo ya kiuchumi.
Hata hivyo Dkt.Bangi
alitoa rai kwa wananchi kuzingatia Mpango wa Nyota ya Kijani ambao umelenga
kuwahimiza wananchi kutumia mpango wa uzazi sanjari na kuboresha upatikanaji wa
huduma hizo kwa wananchi.
Miongoni mwa
faida za uzazi wa Mpango ni pamoja na kuokoa maisha ya akina mama wakati wa
ujauzito na wakati wa kujifungua kwa wastani wa asilimia 40, huku ukisaidia
kupunguza vifo vya watoto wadogo wachanga.
Naibu waziri
wa Afya Mh.Kebwe Steven Kebwe anatarajiwa kuzindua mpango huo wa Nyota ya
Kijani kwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa hiyo kesho katika Uwanja wa Nyamagana ambapo
huduma mbalimbali za uzazi wa mpango zitatolewa huku zikitanguliwa na
maandamano yatakayoanzia katika Hospital ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure kuanzia
majira ya saa mbili za asubuhi.
No comments: