Wadau wa Elimu ya Biashara wakiwa katika majadiliano ya namna ya ujenzi wa Chuo cha CBE Tawi la Mwanza unavyopaswa kuwa.Wadau hawa walikutana jana katika Ukumbi wa Hotel ya JB Belmont.
Chuo cha Elimu ya Biashara CBE Tawi la Mwanza kinatarajia kuanza
ujenzi wa Majengo yake mapya kuanzia mwezi July mwaka huu, kwa lengo la kupanua
wigo wake wa utoaji wa elimu ya biashara hapa nchini.
Mkurugenzi wa Chuo hicho Eustance Joel Mukayu ameyasema hayo hii jana
Mkoani Mwanza baada ya kukutana na wadau mbalimbali wa elimu Mkoani Mwanza kwa
lengo la kujadili mipango na maelengo yatakayofanikisha ujenzi huo kukamilika
kama ilivyokusudiwa.
Mukayu amebainisha kuwa kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaomba
kujiunga na elimu ya biashara katika chuo hicho kuwa kubwa, Uongozi wa Chuo
hicho umeazimia kupanua wigo wake kwa kujenga majengo yake ambayo yatakuwa na
uwezo wa kuchukua wanafunzi wengi zaidi. Tazama picha na Soma maelezo yake pia. |
No comments: