KWELI WATANZANIA HAWAPENDI UNAFKI, TAZAMA KILICHOJILI KATIKA MAZISHI YA MZEE SMALL LINGANISHA NA WANACHOKISEMA BAADA YA KIFO CHAKE.
Ni msiba wa 4 mfululizo ndani ya mwezi mmoja kutoka tasnia ya filamu Tanzania,Jioni ya leo June 09 Said Ngamba au Mzee Small amezikwa na mazishi yake kuhudhuriwa na watu mbalimbali wa serikali,vyama,wasanii na wananchi wa kawaida.
Miongoni mwa watu ambao walihudhuria ni pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete,ilianza kusomwa dua nyumbani kisha baada ya dua kukamilika ilianza safari ya kuelekea kwenye makaburi ya Segerea sehemu ambayo aliomba mwenyewe Mzee Small kuwa kama akifa azikwe hapo.
Hizi ni baadhi ya picha za mazishi ya Mzee Small.
Picha:Global Publishers.
Sasa baada ya kujionea picha hizo, haya ni maoni yaliyotolewa kwenye mitandao ya kijamii...
Eliakimu Solomon · University of Dar es Salaam
binadam
tuna mioyo ya ajabu sana.,mzee small ameugua muda mrefu hakuna
aliyepeleka msaada, leo amefariki umati unatirirka na mbwembwe nyingi
ili muonekane,.laiti angefungua macho awaone sijui mngejificha wapi na
unafiki wenu..R.I.P mzee small
waswahili bana shida tupu sasa wameenda kwenye msiba au wameenda kugombea kushikana mkono na mh Rais.
Mtanzania Media: Pumzika kwa Amani Mzee Small
No comments: