LIVE STREAM ADS

Header Ads

MAKAMU WA RAIS ATOA PONGEZI ZAKE KWA COCACOLA JIJINI MWANZA. AWAASA NA WENGINE KUIGA MAZURI HAYA KUTOKA COCACOLA.

Katika kuadhimisha siku ya Mazingira duniani iliyoadhimishwa kesho, huku Kitaifa maadhimisho hayo yakifanyika katika Uwanja wa Furahisha Mkoani Mwanza, Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal amekipongeza Kiwanda cha Nyanza Bottling Company ambacho kinazalisha vinywaji jamii ya Cocacola kwa kuzingatia Uzalishaji usiohatarisha Uhifadhi wa Mazingira.

Dkt.Bilal aliyasema hayo alipotembelea kiwanda hicho ili kujionea namza shughuli za uzalishaji zinavyofanyika katika kiwanda hicho.Baada ya kujionea namna kiwanda hicho kilivyo rafiki wa mazingira, alivitaka viwanda na wazalishaji wengine kuiga mfano wa Nyanza Bottling Company katika kuzingatia uzalishaji usioathiri mazingira.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Mwanza na wa Kiwada cha Cocacola, wakati alipowasili kwenye Kiwanda hicho kwa ajili ya kutembelea na kujionea mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, jana Juni 5, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Msimamizi Mkuu wa ubora wa Mazingira na Usalama Kazini, Peter Simon, kuhusu jinsi wanavyo tunza mazingira kwa kutotupa maji machafu ambayo hutengenezwa na kuwa masafi na kutumika upya kwa baadhi ya shughuli za kiwandani hapo kama kumwagia bustani, kuoshea magari na n.k.

No comments:

Powered by Blogger.