LIVE STREAM ADS

Header Ads

MICHEZO: HAPA NDIPO TUNAPOANZA KUTOFAUTIANA VIWANGO VYA SOKA.

Wanetu wakiwa katika harakati za kutengeneza mpira kwa ajili ya mchezo wa Mpira wa Miguu.Kwa asilimia kubwa wanetu wa kiafrika hili ni suala ambalo liko juu yao na wanafanikiwa kutokana na juhudi zao.
Baada ya Mpira (Sembo) Kukamilika wanetu huanza mara moja kujifua kwa ajili ya mechi za Kirafiki.Kwa style hii kweli akina Messi wanaweza kupatikana kweli?
Kwa wanetu wa mbele, mtoto hata hajui sembo ni nini wala inavyotengenezwa.Wao kitu kinatoka kiwandani na wanakabidhiwa kwa ajili ya mazoezi tena chini ya ukufunzi wa hali ya juu.
Na hivi ndivyo wanetu wa mamtoni wanavyoandaliwa kimichezo. Ukitafakari Picha zote utagundua namna ambavyo hatufanani hata kidodo, hivyo usishangae kuona namna ambavyo tumekuwa tukifanya katika Soka.Hapa ndipo tunapoanza kutofautiana, Tazama maandalizi yetu (picha za Kinongo) linganisha na hizi za Ulaya utaona utofauti.

No comments:

Powered by Blogger.