Rose Malo ambae ni Afisa Elimu ya Mpiga Kura.
Kutokana na mabadiliko hayo, vituo vya kujiandikishia vimeongezeka
kutoka 24, 919 hadi kufikia 40,015 jambo ambalo litapunguza malalamiko ya
umbali wa vituo vya kujiandikishia na hivyo kuongeza mwamko kwa wananchi kujitokeza
kujiandikisha na kupiga kura.
Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Uchaguzi Kutoka NEC Clotilda
Komba ameeleza kuwa zoezi hilo la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga
kura linahusisha Uandikishaji wa Wapiga Kura wapya ambao ni raia wa Tanzania
waliotimiza umri wa miaka 18 na kuendelea na wale ambao kutokana na sababu
mbalimbali hawakuweza kujiandikisha hapo awali.
|
No comments: