"Bank ya Posta nchini inatoa huduma mbalimbali za Mikopo kwa riba nafuu ikiwa ni pamoja na Mikopo kwa ajili ya Biashara ambayo hutolewa kwa wafanyabiashara ya Kati na Kubwa, Mikopo Midogo Midogo kwa ajili ya Baba/ Mama ntilie, wenye biashara ndogo ndogo kama machinga nk. ambapo aina hii pia hutolewa kwa mtu mmoja mmoja ama vikundi vidogo vidogo. Pia aina nyingine ya Mkopo ni ile ya Mikopo binafsi kwa ajili ya wafanyakazi ama waajiriwa ambayo hutolewa kwa masharti nafuu kabisa na kubwa zaidi ni aina mpya kabisa kwa ajili ya Wastaafu ambapo hutolewa kwa wastaafu". |
No comments: