JIJI LA MWANZA LAJIPANGA KUKABILIANA NA ONGEZEKO LA UCHAFU.
![]() |
Afisa Afya Jiji la Mwanza Danford Kamanya. |
Hii ni
kutokana na kuwepo kwa ongezeko kubwa la uzalishaji wa taka ngumu katika maeneo mbalimbali jijini hapa na swala ambalo litasababisha maeneo
yaliyotengwa kwaajili ya kuwekwa taka kujaa haraka.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake Afisa
Afya Jiji Danford Kamanya alieleza kwamba kutokana na kuwepo kwa
uzalishaji huo, Halmashauri ya jiji kwa kushirikiana na wazabuni mbalimbali,
imeongeza idadi ya magari ya utoaji taka katika maeneo yaliyotengwa ili
kuhakikisha Jiji linaendelea kuwa safi kwa
miaka ijayo .
Alieleza
kuwa magari hayo yataongeza utendaji kazi wa kusafisha mazingira ikiwa ni
pamoja na kuepuka ukaaji wa takataka kwa muda mrefu kwenye maeneo ya
ukusanyaji yaliyotengwa na Halimashauri
ya Jiji.
“Jukumu la
ukusanyaji wa taka Jijini hapa
umeboreshwa kwa ushirikiano wa Halmashauri
na wazabuni ,hivyo kuondokana na
adha iliyopo” Alisema Kamanya.
Na: Prisca Japhes
No comments: