KOMBE LA MEYA JIJINI MWANZA KUANZA KWA MBWEMBWE. PEPSI YAMWAGA VIFAA UTADHANI NI LIGI KUU VILE.
Zoezi la ugawaji wa vifaa kwa timu 22 zitakazoshiriki kwenye mashindano ya Pepsi
Kombe la Meya kwa mwaka huu wa 2014 limefanyika hii leo kwenye uwanja mkongwe
wa Nyamagana jijini Mwanza.
Kila timu imekabidhiwa seti moja ya jezi na mipira miwili
kwenye zoezi ambalo limesimamiwa na wadhamini wa mashindano hayo kampuni ya SBC
kupitia kinywaji cha Pepsi na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya jiji la Mwanza
Stanslaus Mabula.
Mashindano hayo ambayo kwa mwaka huu yanafanyika kwa mara
ya pili yataanzaAugust 2 na kuhitimishwa Septemba 20 huku timu shiriki 22
kutoka halmashauri ya jiji la Mwanza zikiwa zimegawanywa kwenye makundi manne.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya jiji la Mwanza,Stanslaus Mabula amesema kuwa mashindano hayo yatumike katika kuinua vipaji
vya wachezaji huku akiahidi kuwa timu zitakazofika robo fainali pia zitapewa
vifaa vingine.
Mabula ametoa onyo kwa timu au mchezaji atakayeonyesha
utovu wa nidhamu kwa kusema kuwa adhabu zitatolewa huku akisisitiza kamati ya
mashindano hayo itakuwa makini katika kuhakikisha wachezaji mamluki hawachezi.
Bingwa kwenye Pepsi Kombe la Meya mwaka huu atapata zawadi
ya bajaji ya kisasa ya mizigo,TSH.Milioni 1.5,Kombe na medali ya dhahabu huku kitu pekee zaidi mwaka huu ni kutumika
kwa waamuzi wanafunzi wa Alliance School Sports Academy.
“Lengo
kubwa la mashindano haya ni kuwezesha vikundi vya vijana wajasiriamali,
kuleta umoja, hamasa, kuendeleza vipaji vya soka, mshikamano na
burudani, lakini pia kuviwezesha mitaji ya kuendesha shughuli zao
kupitia mashindano ya soka ili kuvijengea uwezo,”
Zawadi
kwa washindi mwaka huu zimeongezeka ambapo bingwa atajinyakulia Bajaji
ya kisasa ya kubeba mizigo na watu wanne yenye thamani ya milioni 4.5 na
fedha tasilimu milioni 1.5 (jumla milioni sita), mshindi wa pili
milioni 2, mshindi wa tatu milioni 1 huku mfugaji bora, timu yenye
nidhamu na mwamuzi bora kuzawadiwa Sh. Laki mbili.
Timu zitakazoshiriki michuano hiyo
zimegawanywa katika makundi manne ambapo kundi A litakuwa na timu sita,
kundi B, C na D kila moja litakuwa na timu tano, mzunguko wa kwanza
utachezwa kwa mtindo wa ligi katika makundi na hatua ya robo fainal timu
zitacheza kwa mtoano hadi kupata timu mbili zitakazo cheza fainali ili
kumpata bingwa kwa mwaka 2014.
“Viwanja
vitakavyotumika katika michuano ya Kombe hilo ni Nyamagana, Nyegezi
Kona, Mabatine Polisi, Buhongwa, Igoma Mnadani na Mkolani na waamuzi
watakaochezesha mashindano hayo ni vijana wanafunzi kutoka katika Kituo
cha Michezo cha Alliance cha jijini hapa,” alieleza mratibu wa mashindano hayo upande wa kanuni Mohamed Bitegego.
Moja
kati ya kanuni za mashindano ya Pepsi Kombe la Meya 2014, zinaeleza
kuwa timu itaruhusiwa kusajili wachezaji wasiozidi 25 kwa fomu
zilizotolewa, Wachezaji wa Ligi kuu ya Vodacom na Ligi Daraja la Kwanza
hawataruhusiwa katika mashindano haya.
Ni kosa kumchezesha mchezaji ambaye hajasajiliwa. Timu itakayo mchezesha mchezaji ambaye hayupo kwenye orodha ya wachezaji waliosajiliwa itapoteza michezo yote ambayo mchezaji huyo aliichezea.
Mchezaji hatoruhusiwa kusajiliwa kwenye timu zaidi ya moja. Iwapo mchezaji huyo akibainika ataondolewa kwenye mashindano na timu hiyo haitoruhusiwa kuweka mchezaji mwingine mbadala, timu itanyang'anywa pointi kwa michezo aliyo cheza mchezaji huyo.
Ni kosa kumchezesha mchezaji ambaye hajasajiliwa. Timu itakayo mchezesha mchezaji ambaye hayupo kwenye orodha ya wachezaji waliosajiliwa itapoteza michezo yote ambayo mchezaji huyo aliichezea.
Mchezaji hatoruhusiwa kusajiliwa kwenye timu zaidi ya moja. Iwapo mchezaji huyo akibainika ataondolewa kwenye mashindano na timu hiyo haitoruhusiwa kuweka mchezaji mwingine mbadala, timu itanyang'anywa pointi kwa michezo aliyo cheza mchezaji huyo.
Mashindano
yatasimamiwa na Kamati ya Mashindano ambayo inamamlaka ya kuifuta
katika mashindano timu yoyote ambayo wachezaji wake watakuwa ni chanzo
cha vurugu katika mashindano.
Mwanzilishi wa Mashindano ya Kombe la Meya, Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza ambae pia ni diwani wa Kata ya Mkoalani (CCM). |
Maamuzi ya refa yatakuwa ya mwisho katika mchezo.
Ni kapteni wa timu pekee ndiye anaruhusiwa kupeleka malalamiko kwa muamuzi ndani ya mchezo.
Timu itakayogomea mchezo itakuwa imepoteza mchezo husika na Kamati ya mashindano itakaa kuijadili timu hiyo kwa adhabu nyingine kama itaona inafaa.
Mchezo utaanza saa 10:30 jioni. Kila timu inatakiwa kufika uwanjani saa moja kabla ya mchezo kuanza.
Viongozi wa timu watatakiwa kusaini kwenye nakala ya kanuni itakayobaki kwa muandaaji wa mashindano ikiwa ni ishara ya kuwa wamezielewa na wataziwasilisha vyema kwenye timu zao ili kuboresha mchezo.
Timu zote 22 zinazoshiriki Mashindano hayo leo zimepokea Vifaa kwa ajili ya Mashindano hayo. |
Na: George Binagi @99.Metro FM & Mtanzania Media Blog, kwa ushirikiano na Gsengo Blog na Issack Wakuganda.
No comments: