Yapo
mambo mengi ambayo yanaweza kukupita katika maisha yako lakini usijutie
hata siku moja. Lakini pia yapo mambo ambayo yakikupita lazima ujutie,
na mambo hayo mara nyingi ni yale yanayotokea mara moja baada ya muda
mrefu/ si mambo ya mara kwa mara...Sasa uzinduzi wa Mixtape ya Rise and
Shine ya Msanii Lil Stiggar ni moja ya matukio ambayo hutakiwi kukosa
maana utajuuu......Utajuuu....Malizia mwenyewe.
Rise and Shine Mixtape ni Kanda Mseto ya
Mwanamziki Lil Stiggar inayosubiriwa na Mamilioni ya Watanzania, ambayo
imebebwa na vionjo mbalimbali vyenye kukonga nyoyo za mashabiki lukuki.
Dhahiri
Shairi muziki unadaiwa kuwa ni moja ya Tiba kwa wagonjwa bada ya
watafiti kadhaa nchini Marekani kuwaweka wagonjwa 100 katika chumba
chenye muziki na wengine 100 kupelekwa hospitalini, lakini waliowekwa
katika chumba maalumu chenye muziki walionekana kupona mapema, kwa
mantiki hiyo basi kanda mseto ya RISE & SHINE ya LIL STIGGAR ni dozi
tosha.
Mwanamziki LIL STIGGAR ni msanii anaetokea
Kundi la Umoja wa Wasanii wa Kike nchini Tanzania liitwalo FeMCTZ ambalo
linaundwa na wasanii wengine kama vile Cindy Rulz, Stosh, Tamy, Tiffer,
Natty E na Kiongozi wao Chiku K.
Kuhusu Kanda Mseto ya
Rise anda Shine ya Lil Stiggar ni kwamba itakuwa na jumla ya Nyimbo
Saba na Bonus Trucks, sanjari na Shows mbalimbali alizowahi kuzifanya
Lil Stiggar, video/nyimbo zake, lylics pamoja na Biography yake ambavyo
vyote kwa pamoja vitakuwa katika mfumo wa DVD.
Wasanii
walioshirikishwa katika Kanda Mseto hiyo ni pamoja na Phyno, Ammy Chiba,
Gest Lydar, Chris Daniel, Ottuck, Zax B, Sauti from East na Anno
Melody. Maprodyuza waliohusika kuitengeneza Rise and Shine Mixtape ni
Phyno Touchz, Dayo Music, MG Creator, Losso Touchez, Gach, Nachi &
Waisa, Kingston na Kebby.
Uzinduzi wa Rise and Shine
utafanyika Agost 02 Mwaka huu Jiji Mbeya katika Ukumbi wa Mtenda Sunset
Conference kwa Kiingilio cha Shilingi 10,000 ambapo tiketi zimeanza
kuuzwa hivyo wahi mapema kununua tiketi yako mapema kupitia Simu namba
0654 07 99 30.
Uzinduzi huo utasindikizwa na Wasanii kibao huku Red Carpet,
Dancing na Maonyesho ya Mavazi ya Kiafrika yaliyopewa jina la "SONDELA".Uzinduzi huu umedhaminiwa na Bomba FM Radio, Mbeya FM, The
Premier Show ya G FM, Life Parners Ent, Sweet FM, Highlands FM, T Motion
Films, Elishadai Records, Native Films, Chimbuko letu Blog na Kuletwa
kwenu na Mtanzania Media Blog.
NB: Unaweza Like page ya
Lil Stiggar kupitia facebook kwa jina hilo la LIL STIGGAR na Instagram
kupitia jina hilo pia la LILSTIGGAR.
Na: Greyson Salufu Chatanda a.k.a Chris Bee-Mbeya. |
No comments: