Waimbaji hawa wako Mkoani Mwanza kwa ajili ya Kuhudumu katika Mkutano Mkubwa wa Injili Unaofanyika katika Uwanja wa Furahisha Wilayani Ilemela. Mkutano huu ulianza tangu Jumapili ya wiki iliyoisha ya June 29 na unatamatishwa hii leo July 06. Katika Mkutano huo, mbali na huduma ya Uimbaji pia Masanja anahudumu kama mchungaji hivyo kama jana jumamosi hukumshuhudia akihubiri katika Uwanja wa Furahisha, basi leo hutakiwi kukosa kwa kuwa Masanja atakuwa akihudumu katika Mkutano huo. Pia mwimbaji Flora Masha nae atakuwepo katika Mkutano huo. |
No comments: