Akizungumza katika Mkutano huo, Wenje amebainisha kuwa yeye hakatai
Machinga kuondolewa katika Maeneo ambayo hayaruhusiwi kisheria katikati ya Jiji
la Mwanza, isipokuwa anapingana na namna Operesheni hiyo inavyoendeshwa ambapo
Mgambo wa Jiji wamekuwa wakiwanyanyasa Wafanyabiashara hao pindi wanapokuwa
wakitekelezwa Operesheni hiyo.
“Mimi Msimamo wangu sijakaa watu waondolewe Nyerere Road na Kenyatta
Road, lakini hii Operesheni izingatie Ubinadamu..kwa nini Polisi apige mtu? Mtu
anakamatwa anapigwa, Kuna mwanamke juzi nimeambiwa amekamatwa amepigwa
kwelikweli na polisi…mpaka migambo, migambo wanatuzingua wakati jioni wanalala
kwao bila bunduki…hata hawa polisi hawatembei na bunduki...kwa hiyo ninachosema
tunahitaji amani iwepo katika huu mji…kwa hiyo hatuhitaji mwananchi hata mmoja
anyanyaswe… ” Alisema Wenje.
|
No comments: