Soko la Bugarika lililoko Wilayani Nyamagana Mkoani Mwanza limewaka Moto Usiku huu (Jumamosi) majira ya saa nne na kuteketeza baadhi ya Bidhaa na Mali za Baadhi ya Wafanyabiashara wanaofanya biashara zao katika Soko hilo.Chanzo cha Moto huo kimeelezwa kuwa ni Shoti ya Umeme huku taarifa kutoka jeshi la zima Mototo Mkoani Mwanza zikieleza kuwa ni Mlipuko uliotokana na Mafuta ya Petrol yaliyokuwa yakiuzwa katika duka lililokuwa jirani na soko hilo na juhudi za kuuzima moto huo zimefanikiwa kwa ushirikiano na wananchi pamoja na Kikosi cha Zima Moto na hivyo kusaidia kuuzima moto huo.Hakuna madhara makubwa yaliyosababishwa na moto huo kwa kuwa mali nyingi zimeokolewa katika soko hilo japo watu wawili (Mtu na Mke wake, wamiliki wa duka) waliokuwa katika duka ambalo moto ulianzia wamejeruhiwa na wamekimbizwa katika hospital ya Bugando kwa ajili ya matibabu. |
No comments: