ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUCHOMWA KISU TUMBONI. UTUMBO NUSRA UMWAGIKE NJE.
![]() |
Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza SACP. Valentino Mlowola. |
Bernald
Otieno (26) mkazi wa butimba kona mtaa wa Magereza Mkoani Mwanza, amenusurika
kifo baada ya mzazi mwenzake Martha Gabriel (32) kumchoma kisu tumboni.
Tukio hilo lilitokea
juzi jumanne saa
nne usiku huko butimba ambapo Benard alidai kuwa alienda kwa ndugu zake Mtaa wa
Igogo siku ya jumapili kusalimia, akachelewa kurudi nyumbani kutokana na
usafiri usiku huo ulikuwa wa shida akurudi nyumbani jumatatu.
Alisema kuwa siku hiyo
alinimtaarifu mzazi mwenzake amekosa usafiri lakini hakumjibu kitu na siku ya
jumatatu usiku alishangaa kuona mzazi mwenzake amekusanya nguo zake kwa lengo
la kutaka kuondoka nyumbani hapo.
‘’usiku huo tulikuwa tumelala na
ghafla Martha aliamka na kuchukuwa kisu na kasha kunichoma tumboni ndipo nilijaribu
kupambana nae na hatimae nikafanikiwa kutoka nje kwa lengo la kuomba msaada kwa
majirani ambapo yeye nilimfungia mlango kwa nje ili asitoke’’. Alisema
Otieno.
Aliongeza kuwa Martha si mara yake ya kwanza kumfanyia kitendo cha kikatili na kipindi cha nyuma wakiwa wanaishi Mkoani Tabora aliwahi kumwagia mafuta ya diesel na kumchomea nyumba alipokuwa amelala na watoto wake.
Mweyekiti wa mtaa huo Abeid Musa akizungumzia suala hilo amesema kuwa alisikia mtu anapiga kelele ya kuomba msaada na walipofika walimkuta Otieno kashikilia utumbo huku analia na hivyo wakamchukua na kumpeleka hospital ya Rufaa Bugando kwa ajili ya Matibabu zaidi.
Aliongeza kuwa Martha si mara yake ya kwanza kumfanyia kitendo cha kikatili na kipindi cha nyuma wakiwa wanaishi Mkoani Tabora aliwahi kumwagia mafuta ya diesel na kumchomea nyumba alipokuwa amelala na watoto wake.
Mweyekiti wa mtaa huo Abeid Musa akizungumzia suala hilo amesema kuwa alisikia mtu anapiga kelele ya kuomba msaada na walipofika walimkuta Otieno kashikilia utumbo huku analia na hivyo wakamchukua na kumpeleka hospital ya Rufaa Bugando kwa ajili ya Matibabu zaidi.
Muuguzi kiongozi wa wodi Ester
Pastor aliyempokea Otieno alisema kuwa kisu alichokuwa amechomwa kilikuwa
kimepita hadi kwenye utumbo mwembamba hivyo ilibidi wamfanyie upasuaji na kwa
sasa hali yake inaendelea vizuri.
Kamanda wa Polisi Mkaoni
hapa SACP. Valentino Mlowola alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na
amebainisha kwamba mtuhumiwa huyo amekamatwa na atafikishwa mahakamani muda
wowote upelelezi utakapokamilika ili kujibu shitaka linalomkabiri.
Na Prisca Japhes: Mtanzania Media-Mwanza.
No comments: