SEKTA YA MADINI INAKUA HAPA NCHINI. LAKINI INACHANGIA ASILIMIA KIDOGO KATIKA PATO LA TAIFA.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi
Evarist Ndikilo amebainisha kwamba Sekta ya Madini imeendelea kukua hapa
nchini, japo bado sekta hiyo ina changamoto mbalimbali ambazo ni pamoja na
kuchangia pato kidogo katika Uchumi wa Taifa.
Hayo yamebainishwa
hii leo katika taarifa yake iliyosomwa na
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndaro Kulwijira, wakati akifungua Mkutano wa
Wadau wa Madini Mkoani Mwanza uliofanyika katika Ukumbi wa Gold Crest Hotel.
Amesema kuwa
Sekta ya Madini imeendelea kukua kadri siku zinavyozidi kwenda, japo inakabiliwa
na baadhi ya changamoto kama vile kuchangia kidogo katika pato la Taifa
ikilinganishwa na sekta zingine.
Aidha
amebainisha kuwa Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita Sekta ya Madini imekuwa
kwa wastani wa asilimia 10.42 hii ikiwa ni kati ya mwaka 2002 na 2012 huku
ikikadiriwa kwamba ifikapo mwaka 2025 Sekta ya Madini itaweza kuchangia katika
pato la Taifa kwa takribani asilimia 10 ikilinganishwa na asilimia 3.3 ya hivi
sasa.
Akizungumza
nje ya Ukumbi wa Mkutano huo, Ndaro amebainisha kuwa mchango wa Sekta ya Madini
kwa hivi sasa ni mdogo licha ya sekta hiyo kuonekana kukua kutokana na ukwepaji
wa ulipaji wa kodi unayotokana na biashara ya madini ikiwa ni pamoja na
usafirishaji wa madini nje ya nchi kwa njia za panya, ambapo ameshauri kuwa ili
kuondokana na hali hiyo ni vyema wadau wote wa sekta ya madini wakatambulika na
kufanya shughuli zao katika mfumo ulio rasmi.
Mhandisi Ally Samaje ambae ni Kamishna Msaidizi wa Ukaguzi wa Migodi. |
Akizungumza
kwa niaba ya Kamishna wa Madini nchini, Mhandisi Ally Samaje ambae ni Kamishna
Msaidizi wa Ukaguzi wa Migodi amebainisha kwamba lengo la Mkutano huo ni
kujadili utekelezaji wa utumiaji wa huduma mbalimbali zinazotakiwa katika migodi
hapa chini kama sera ya Madini ya Mwaka 2009 inavyoelekeza.
Amesema sera hiyo inayaelekeza makampuni ya madini yanayopatikana hapa nchini kutumia huduma na maduduzi yote ambayo yanapatikana nchini bila kuyafuata nje ya nchi sanjari na kuwaajiri Watanzania kwa lengo la kuwezesha sekta hiyo kuchangia katika pato la Taifa bila kutegemea kodi wala mirabaha ya madini pekee.
John Henjewele ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime Mkoani Mara alikuwa Mmoja wa Washiriki wa Mkutano huo. |
Katika hatua
nyingine Samaje amekiri kwamba ni kweli vitendo vya utoroshaji wa madini hapa
nchini upo, japo amefafanua kwamba utoroshaji huo hauyahusishi makampuni
makubwa ya Madini huku akiongeza kuwa Serikali imechukua hatua ya kupambana na
hali hiyo ikiwa ni pamoja na kuweka wakaguzi katika maeneo yote ya upitishaji
wa Madini kwenda nje ya nchi ambayo ni pamoja na viwanja vyote vikubwa vya
ndege hapa nchini.
Amebainisha
kuwa utoroshaji wa Madini uliopo kwa hivi sasa hapa nchini ni ule unaotokana na
uuzwaji wa madini kiholela kutoka kwa wachimbaji wadogo wadogo ambao wanawauzia
wageni madini hayo mitaani bila kufuata taratibu zilizopo.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndaro Kulwijira. |
Baadhi ya Wadau walioshiriki katika Mkutano huo. |
Mkutano huo wa Wadau wa Madini
umelenga kujadili utekelezaji katika Sekta ya Madini katika kulinufaisha Taifa,
kwa kuangalia hali ilivyo kwa hivi sasa na wapi kuna changamoto katika Sekta
hiyo kukuza uchumi wa Taifa ili kupata majibu yatakayosaidia ukuaji wa sekta
hiyo sambamba na ukuaji wa pato la Taifa.
Na: George Binagi @99.4 Metro FM & Mtanzania Media.
No comments: