VYOMBO VYA HABARI MKOANI MWANZA LAWAMANI.
![]() |
Mwenyekiti wa kikundi cha Kirumba Sanaa, Issa Katumba. |
Akizungumza Wiki hii, Mwenyekiti wa kikundi cha Kirumba Sanaa Kilichopo Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza, Issa Katumba alisema wadhamini wamekuwa wakishindwa kudhamini tamthilia zenye kuelimisha hivyo wamekuwa wakitoa kipaumbele kwa vitu ambavyo havielemishi jamii.
Hata hivyo alisema mpaka
sasa wameisha kamilisha tamthilia ya Malimwengu itakayoanza kuonyeshwa kupitia
vituo mbalimbali vya televisheni nchini na kuingizwa kwenye king`amzi cha
Continetal namba 107 ili kuhakikisha watanzania wanajifunza.
“Hii tamthilia ina
maudhui ya kitanzania ambayo mtazamaji atakae pata nafasi ya kuiona atajifunza
mambo mengi ya mila na desturi za mwafrika anavyotakiwa kuishi na ninawaomba
watanzania wenzangu kuutuunga mkono. Alisema Katumba na kuongeza
“Tamthilia hii imechezwa
na wasanii chipukizi kutoka mkoa wa Mwanza, Kalenga Kiokote ambaye amecheza
kama muhusika mkuu katika tamthia hiyo ambapo aliigiza kama kama mtoto wa
mtaani alionesha uwezo mkubwa sana na ambae anahitaji kusaidia,” alisema
Katumba.
Na: Prisca Japhes, Mwanza.
![]() |
Mwenyekiti wa kikundi cha Kirumba Sanaa, Issa Katumba. |
No comments: