LIVE STREAM ADS

Header Ads

WASHIRIKI MISS LAKE ZONE 2014 WATEMBELEA SHULE YA AWALI NA MSINGI RISHOR ILIYOKO MISUNGWI MKOANI MWANZA. MKURUGENZI WA SHULE AFUNGUKA.

Jumla ya Washiriki 18 wa Miss Lake Zone wakiwa katika Picha ya Pamoja na Wanafunzi wa Shule ya Awali na Msingi Rishor pamoja na Mkurugenzi Mkuu (Me) sanjari na Mkurugenzi Mtendaji (Ke).
Wadau mbalimbali wameshauriwa kujitokeza kuwekeza katika huduma mbalimbali za kijamii ambazo ni pamoja na Elimu sanjari na Afya, kwa lengo la kusaidia katika kuihudumia jamii kwa kuwa bado huduma hizo upatikanaji wake ni wa kusua sua hapa nchini.

Ushauri huo umetolewa hii leo Mkoani Mwanza na Leus Kibona ambae ni Mkurugenzi Mkuu wa Shule ya Awali na Msingi Rishor iliyoko Tarafa ya Usagara Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza, baada ya kutembelewa na Washiriki wa Shindano la Urembo Kanda ya Ziwa, Maarufu kama Miss Lake Zone 2014.

Kibona alibainisha kuwa bado sekta ya elimu inasua sua hapa nchini hivyo ni vyema watu wenye uwezo wakawekeza kwenye elimu kwa kujenga shule na vyuo mbalimbali vya elimu kwa lengo la kusaidia upatikanaji wa elimu sanjari na kuinua kiwango cha elimu hapa nchini.
Aidha aliongeza kuwa huduma za kijamii kama vile Afya pia nazo pia zinahitajika hivyo wadau mbambali wajitokeze kwa aajili ya kujenga vyuo vya Afya na Zahanati ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za Afya katika jamii hapa nchini.

Ili kuonyesha ushiriki wake katika jamii, Shule ya Rishor imeazimia kutoa nafasi mbili kwa wanafunzi walio katika mazingira magumu katika Tarafa ya Usagara kwa ajili ya kuwasomesha bure, huku Mkurugenzi wa Shule hiyo akiahidi kuongeza idadi ya kuwasomesha wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu kadri uwezo wake utakavyokuwa ukiongezeka.

Kuhusiana na Shindano la Redd’s Miss Lake Zone 2014, Shule ya Rishor ni miongoni mwa wadhamni waliojitokeza katika udhamni, ambapo Mkurugenzi wa Shule hiyo aliwasihi washiriki wa Shindano la Miss Lake Zone kuzingania pia suala la elimu ili kuweza kupata uelewa zaidi shughuli zao.
Kwa upande wao Washiriki wa Shindano hilo waliezea furaha yao baada ya kuchaguliwa kuiwakilisha Mikoa yao ya Kanda ya Ziwa, ambapo kila Mkoa umetoa Washiriki watatu kwa ajili ya kujishiriki Shindano hilo la Miss Lake Zone 2014 na hivyo kufanya idadi ya washiriki wa shindano hilo kuwa 18 kutoka Mikoa yote sita ya Kanda ya Ziwa ambapo kiingilio kimepangwa kuwa ni shilingi 5,000, 10,000 na 30,000.

Aidha washiriki hao pia waliishauri jamii ya Watanzania kuwekeza zaidi katika elimu kwa kuwa kiwango cha elimu hapa nchini bado hakiridhishi, huku wakiongeza kuwa wakazi wa Kanda ya Ziwa ikiwemo Mkoa wa Mwanza wajitokeze kwa wingi siku ya Jumamosi Agost 30 katika Uwanja wa CCMK Kirumba ili kushuhudia shindano hilo la Miss Lake Zone 2014.



Kwa Upande wake Flora Lauwo ambae ni muandaaji wa Shindano hilo kupitia kampuni yake ya Flora Promotion alibainisha kuwa, Mshindi wa Kwanza atapata zawadi ya gari yenye thamani ya shilingi Milioni Kumi, Mshindi wa Pili atajipatia zawadi Bajaji yenye tahamani ya shilingi milioni nne, ambapo mshindi wa tatu atapata fursa ya kusomeshwa huku mrembo mwenye kipaji akijishindia zawadi ya pikipiki yenye thamani ya shilingi milioni moja na laki sita sanjari na zawadi mbalimbali kutoka kwa wadhamni.

Nae Benny Mwangi ambae ni Meneja wa Lenny Hotel iliyopo Mkoani Geita, alieleza kuwa Lenny Hotel ilijitokeza kudhamini shindano hilo kwa lengo la kuboresha mashindano hayo, huku akiongeza kuwa jamii inapaswa kubadili mtizamo na kuachana na fikra potofu kuwa mashindano ya urembo ni uhuni. Lenny Hotel katika udhamini wake imetoa zawadi ya gari yenye thamani ya shilingi Milioni kumi kwa ajili ya mshindi wa kwanza

Mtoto huyu alikuwa ni Kivutio cha Mamiss kutokana na namna alivyokuwa akijipanga katika kupiga picha na Mamiss.
Jamani huyu Mtoto ni mcheshi sana. Hapa alikuwa na Anko wake George Binagi-GB Pazzo kutoka Radio Metro, akiwa pia ni Managing Director wa Mtanzania Media.

Warembo wanaoshiriki Redd's Miss Lake Zone wakiwa na Lydia (Katikati) ambae ni Mwandishi wa habari kutoka Radio City FM Jijini Mwanza.

Leus Kibona (katikati) ambae ni Mkurugenzi Mkuu wa Rishor Pre & Primary School akizunguka shuleni hapo hii leo baada ya warimbwende kutembelea shule yake.
Wa kwanza ni Leus Kibona ambae ni Mkurugenzi Mkuu , akifuatiwa na Peris Kibona ambae ni Mkurugenzi Mtendaji, anaefuata aliesimama ni Seleman Mohamed ambae ni Msema, hao ni baadhi ya Viongozi wa Rishor Pri & Primary School na anaefuata aliekaa ni Flora Lauwo ambae ni Mkurugenzi wa Flora Promotion, ambao ni waandaaji wa Mashindano ya Miss Lake Zone 2014.

Warimbwende wanaoshiriki shindano la Redd's Miss Lake Zone 2014
Wanafunzi wa Rishor Pri & Primary school


Ilikuwa Time ya Bites kidogo.
"Kasema nani kuwa Mamiss hawaliiiiiiii" Haya sasa sahani hizo hapo"
Wanafunzi
"Eti Kidoti akawa ananikiss, jamani majaribu mengine me siyawezi"

Flora Lauwo ambae ni Mwandaaji wa Redd's Miss Lake Zone 2014, chini ya Kampuni yake ya Flora Promotion.

Judith Josephat Maturege (Ke) ambae ni Matron wa Mamiis hao.
"Warimbwende"

Baadhi ya Majengo yaliyopo Rishor Pri & Primary School
Jengo la Utawala katika Shule ya Rishor Pri & Primary School likiwa na Vifaa vya Kisasa kabisa ndani yake. Shule hii ni ya Kutwa na Bweni.
Na: George Binagi @99.4 Metro FM & Mtanzania Media.

No comments:

Powered by Blogger.