Warsha ya
Uboreshaji wa Huduma za hali ya Hewa Katika Maeneo ya Ziwa Victoria pamoja na
mambo mengine, pia imejikita katika majadiliano juu ya Mradi wa Majaribio
uliotekelezwa katika Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza, kuhusiana na Utoaji wa
Taarifa za Hali ya Hewa kwa njia ya Simu za Mkononi na umenuiwa kuendelezwa
katika maeneo yote hapa nchini.
Mradi huo ulianza
majaribio yake tangu July 17 mwaka jana, na uliwashirikisha wadau mbalimbali
ambao ni pamoja na Wakulima, Wavuvi, Vyombo vya Habari na wasafirishaji wa
Majini huku ukiwa umelenga kutumia njia ya simu za mkononi kufikisha taarifa za
hali ya hewa kwa wananchi. Warsha hiyo ilianza jana Agost 18 katika Hotel ya
Gold Crest Jijini Mwanza, na inatarajia kufikia tamati kesho Agost 20 mwaka
huu.
|
No comments: