Baada ya
Mradi huo kuonyesha mafanikio, TMA itaweza kuupeleka katika maeneo mbalimbali
hapa nchini, lengo likiwa ni kuhakikisha kwamba taarifa za utabiri wa hali ya
hewa zinawafikia wananchi kwa wakati zaidi.
Aidha TMA
imeshauriwa kuboresha utendaji kazi wake zaidi na wadau wengine wakiwemo
wanahabari, kama daraja la kufikisha taarifa za utabiri wa hali ya hewa kwa
wananchi, huku wananchi nao wakishauriwa kuzifuatilia kwa umakini taarifa za
hali ya hewa zinazotolewa na TMA kwa kuwa hatua hiyo inaweza kuwaepusha na
athari mbalimbali wawapo katika shughuli zao, mfano uvuvi nk.
|
No comments: