Mgomo wa Wafanyabiashara Jijini
Mwanza leo umeingia katika Siku yake ya Pili huku Juhudi za kuhakikisha kuwa
Mgomo huo unafikia tamati zikiwa zinaendelea ambapo mapema hii leo viongozi wa
Jumuia ya Wafanyabiashara Mkoani Mwanza, wamekutana na Uongozi wa Halmashauri
ya Jiji la Mwanza kwa ajili ya Kutafuta suluhu ya Mgomo huo.
Wakati Mgomo
huo Ukiendelea hii leo, Tayari kuna stofahamu miongoni mwa Wafanyabiashara wa
Maduka Jijini Mwanza, ambapo miongoni mwao wapo wanaounga mkono uwepo wa Mgomo
huo, huku baadhi yao wakiwa hawaungi Mkono Mgomo huo na hivyo kuonekana
wakifungua Maduka yao japo kwa tahadhari.
|
No comments: