LIVE STREAM ADS

Header Ads

BABA AMSABABISHIA MWANAE KIFO KUTOKANA NA KIPIGO JIJINI MWANZA. AMFICHA MWINGINE NDANI AKIWA NA MAJERAHA MAKUBWA.

Mwanainchi wa Mtaa wa Mwembeni A Kata ya Pamba Jijini Mwanza wakiwa wamekusanyika nyumbani kwa Mwanaume anaedaiwa kusababisha Umauti mwa mwanae kutokana na kipigo huku mwingine akiwa amefichwa ndani huku akiwa na majeraha makubwa katika sehemu za mwili wake.
Mwanaume mmoja Mkazi wa Jijini Mwanza anatuhumiwa kwa kosa la kusababisha Mauaji ya Mtoto wake, huku mtoto mwingine nae akiwa katika hali mbaya ya majeraha baada ya watoto hao kwa nyakati tofauti kudaiwa kupigwa na mwanaume huo.

Tukio hilo limetokea katika Mtaa wa Mwembeni A katika Kata ya Pamba iliyoyopo Wilaya ya Nyamagana Jijini Mwanza, ambapo mwanaume huyo ambae ni mzazi wa watoto hao anadaiwa kuwa alikuwa na desturi ya kuwapiga watoto hao mara kwa mara kwa madai kwamba si damu yake.

Katika tukio la Kwanza Mwanaume huo ambae ametajwa kwa jina la Mwita au Yusuph anadaiwa kumpiga mtoto wake wa kambo na kumsababishia majeraha katika sehemu mbalimbali za mwili wake hali iliyosababisha mtoto huyo kupoteza maisha akiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure baada ya kumficha mtoto huo nyumbani kwa siku kadhaa bila matibabu.

Mtoto aliefariki kutokana na majeraha yaliyotokana na kipigo kutoka kwa mwaume huyo anafahamika kwa jina la Wambura Yusuph mwenye umri wa miaka miwili, ambae amefariki hii leo akiwa katika Hospital ya Sekour Toure akipatiwa matibabu.

Majirani wakiwa na Majonzi tele baada ya Kupata taarifa ya jirani mwenzao kumpiga mtoto wake hali iliyosabanisha mtoto huyo kufikwa na umauti kutokana na kipigo hicho.

Katika tukio la pili Mwanaume huyo pia, anadaiwa kumpiga mtoto wake mwingine hadi kufikia hatua ya kumchoma moto. Mtoto huyo anafahamika kwa jina la Baraka Mussa mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu na kumsababishia majeraha makubwa katika sehemu za mwili wake hususani magotini na kasha kumficha ndani huku na kuendelea kumtibu kiholela.

Baada ya kupata taarifa hizo, Shirika la kutetea haki za Watoto la Foundation Karibu Tanzania lililopo Mkoani Mwanza kupitia kwa Johanes Emmanuel ambae ni Afisa Ustawi wa Shirika hilo kwa kushirikiana na viongozi wa Mtaa huo waliweza kufika nyumbani kwa Mwanaume huyo kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria sanjari na usaidizi wa mtoto aliekuwa amefichwa ndani akiuguza majeraha.

Hatimae mwanaume huyo alifika nyumbani na kutakiwa kuambatana na viongozi wake wa mtaa kwenda katika kituo cha polisi kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazomkabili, lakini juhudi hizo hazikuweza kuzaa matunda kwani mwanaume huo alifanikiwa kutoroka na kutokomea kusikojulikana.  

Baada ya Mwanaume huo kutoroka, Viongozi wa Mtaa huo wa Mwembeni A waliamua kuondoka na Wake za Mwanaume huyo, ambapo Mke mmoja aliefahamika kwa jina la Christina Mussa (21) ndie mwanae Baraka Mussa (1) alikuwa amefichwa ndani akiwa na majeraha huku Nyangi Yusuph (23) akiwa ndie mwanae Wambura Yusuph (2) amefikwa na umauti.

Afisa Mtendaji Mtaa wa Mwembeni A Prisca Evarist (Kushoto) akiwa na baadhi ya Wakazi wa Mtaa huo nyumbani kwa mwanaume anaedaiwa kutenda ukatili kwa watoto.

Hadi tunakwenda mitamboni Wanawake hao walikuwa wamefikishwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Nyamagana kwa ajili ya kutoa maelezo juu ya matukio hayo, ambapo kwa upande wa majirani wamewatupia lawama wanawake hao kutokana na kuyafumbia macho matukio hayo. Na hapa mama wa Mtoto aliechomwa moto anaeleza jinsi ilivyo kuwa.
                                                        
Kwa pamoja Seleman Nasoro ambae ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwembeni A, Maria Thomas ambae ni Balozi wa Mtaa Mwembeni A pamoja na Prisca Evarist ambae ni Afisa Mtendaji wa Mtaa huo wa Mwembeni A wamelaani kitendo kilichofanywa na Mwanaume huo ambapo wametoa rai kwa wanajamii kutokaa kimya pindi wanapoona matukio ya kikatili katika maeneo yao.

Majirani nao wakaelezea kusikitishwa kwao na Kitendo cha Mwanaume huyo kuwaadhibu watoto wake kikatili huku wakiwatupia lawama wakielekeza lawama kwa wake wote wawili wa mwanaume huyo kwa kitendo cha kukaa kimya bila kulipoti vitendo vya kikatili vilivyokuwa vikifanywa na mwanaume huo.
                                                        
Awali akizungumza juu ya Matukio mbalimbali ya Kikatili wanayotendewa watoto katika Jamii, Abimeleck Richard ambae ni Mwezeshaji na Mwanasheria kutoka Shirika la kutetea haki za watoto lililopo Mkoani Mwanza la Foundation Karibu Tannzania ameishauri jamii kuwa tayari kuchukia vitendo vya kikatili vinavyotokea katika jamii.

Christina Mussa ambae ni Mama wa Mtoto Baraka Mussa ambae ameunguzwa na kufichwa ndani kwa muda mrefu bila matibabu.
Nyangi Yusuph (23) ambae mwanae Wambura Yusuph (2) amefariki baada ya kuuguza kwa siku kadhaa majeraha yanayodaiwa kusababishwa na kipigo kutoka kwa baba yake wa kambo.
Nyangi Yusuph (23) (kushoto) ambae mwanae Wambura Yusuph (2) amefariki baada ya kuuguza kwa siku kadhaa majeraha yanayodaiwa kusababishwa na kipigo kutoka kwa baba yake wa kambo.
Mtoto Yusuph (mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu) akiwa katika hali ya majeraha baada ya kufichwa ndani kwa siku kadhaa.
Hizi ni taarifa za Awali.Endelea kuwa nasi hadi tutakapokuletea taarifa kutoka Mamlaka zinazohusika, kama vile Polisi nk. 
Binagi Media Group, Kwa Pamoja Tuijuze Jamii; Usikae Kimya kwa Tukio lolote lile la kikatili katika jamii yako.Tunahitaji  Familia na Jamii Salama.

No comments:

Powered by Blogger.