MBARONI KWA KUHUSIKA NA UVAMIZI WA KITUO CHA POLISI MKOANI GEITA.
KAMANDA WA POLISI MKOANI GEITA JOSEPH KONYO. |
Kufuatia msako mkali
uliofanywa jana na jeshi la polisi nchini katika Mkoa wa
Geita eneo la Ushirombo wilaya ya Bukombe, Jeshi hilo limefanikiwa
kumkamata mtu mmoja waliyekuwa wakimhisi kuwa ni jambazi ambaye amekutwa akiwa
ameketi juu ya mti huku akiwa ameshikilia bomu.
Mtu huyo ambaye hakufahamika jina lake mara moja alikutwa juu ya
mti majira ya jana jioni wakati msako mkali wa jeshi la polisi ukiendelea
katika eneo hilo ambapo pia jeshi hilo limefanikiwa kupata bunduki saba aina ya
SMG zikiwa zimefichwa kwenye tanuru la kuchomea matofali.
Jeshi
la polisi pia lilimkamata mtu huyo huku likimficha sura yake kwa kitambaa
cheusi baada ya kumhisi kuwa alishiriki kitendo cha mauaji ya askari wawili
waliokuwa zamu katika kituo kidogo cha polisi na watatu kujeruhiwa
huku taarifa zikieleza kuwa askari mmoja aliyekuwa majeruhi alifia njiani
wakati akikimbizwa katika hospitali ya rufaa Bugando jijini Mwanza.
Hata
hivyo jeshi la polisi nchini limetangaza dau la shilingi millioni 10 kwa
mtu yeyote atakaye fanikisha kuwakamata au kuwabaini waliohusika na uvamizi huo
Kituo
kidogo cha polisi kilichopo ushirombo wilayani Bukombe mkoani Geita
kilivamiwa na majambazi usiku wa kuamkia
jana jumamosi saa tisa usiku huku askari
wawili wakiuwawa na watatu wakijeruhiwa
vibaya.
Ambapo
taarifa zilieleza kwamba kuwa majambazi hao walilipua chumba cha kuhifadhia silaha na kufanikiwa kuondoka na silaha zaidi ya tano aina ya SMG.
No comments: