Isaack Wakuganda (Kulia) akiwa na Sefroza Joseph wakati wakifanya kazi wote Radio Metro.
“Tarehe
03/09/2014 siku ya jumatano, nimeacha rasmi kazi ya utangazaji wa Michezo
-Radio Metro FM ya Mwanza. Nimekitumikia kituo hicho kwa miaka mitatu toka
mwaka 2011. Nawashukuru sana viongozi wa vyama vya michezo mbalimbali wa
kitaifa, Mkoa wa Mwanza na Mikoa yote ya kanda ya ziwa bila kusahau viongozi wa
vilabu vya soka Mkoani Mwanza kwa ushirikiano wao walioutoa kwangu. Sitawasahau
wasikilizaji wangu, nawathamini sana. Michezo naipenda sana na hivyo nitaendelea
kuwa mwanamichezo”. Alisema Wakuganda ambae wengi wanamfahamu kama Libero
asiechoka anapokuwa dimbani.
Hatua
hiyo ya Wakuganda kuacha kazi imeonekana kuwashtua watu wengi ndani na nje ya
Jiji la Mwanza si tu kwa wasikilizaji wa Radio Metro bali hata pia takribani viongozi
mbalimbali wa Vyama Soka hapa nchini ambao alikuwa akishirikiana nao kwa
ukaribu zaidi.
|
No comments: