WANANCHI MWANZA WAHIMIZA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Makundi mbalimbali ya wananchi jijini Mwanza yamejitokeza kwa wingi na kushiriki kongamano la kuhamasisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.
Kongamano hilo limeandaliwa na makundi hayo ambayo ni pamoja na machinga, bodaboda, wamiliki wa daladala, mama lishe na watu wenye ulemavu chini ya mlezi wao, Stanslaus Mabula ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo la Nyamagana kwa awamu mbili kuanzia mwaka 2015/ 20225.
Akizungumza kwenye kongamano hilo lililofanyika Jumamosi Oktoba 25, 2025 katika uwanja wa Nyamagana, Katibu wa wamiliki wa daladala Mkoa wa Mwanza, Hussein Mosha amesema Mwanza wamejiandaa kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa amani na utulivu.
"Niwaombe kila mmoja tuendelee kudumisha amani ya nchi yetu, bila amani hata pikipiki zetu hatuwezi kuziendesha, amani yetu ndiyo maisha yetu" amesema Mwenyekiti wa waendesha bodaboda Mkoa wa Mwanza, Mohamed Idd akihimiza wananchi kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa amani.
Naye Katibu wa Machinga Mkoa wa Mwanza, Zuena Mahamudu amewahimiza wananchi kuepuka vitendo vya uvunjifu wa amani wakati wa uchaguzi na badala yake wakashiriki zoezi la kupiga kura kwa wingi kwa mstakabali wa maisha yao.
Kwa upande wake mlezi wa makundi maalum ya wananchi walioandaa kongamano hilo, Stanslaus Mabula ambaye ni mbunge wa Nyamagana aliyemaliza muda wake amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi Oktoba 29, 2025 kupiga kura kwa amani ili kuwachagua viongozi bora watakaowavusha kimaendeleo.
Na George Binagi, BMG Media
Katibu wa wamiliki wa daladala Mkoa wa Mwanza, Hussein Mosha akihimiza wananchi kulinda amani wakati wa Uchaguzi Mkuu 2025.
Katibu wa Machinga Mkoa wa Mwanza, Zuena Mahamudu akizungumza kwenye kongamano hilo na kuhimiza wananchi kujitokeza kwa amani kupiga kura.
Mwenyekiti wa madereva wa daladala Mkoa wa Mwanza, Mjarifu Manyasi akihimiza wananchi kujitokeza kwa amani kushiriki uchaguzi Oktoba 29, 2025.
Mwenyekiti wa Muungano wa Machinga Mkoa wa Mwanza, Said Tembo akihimiza amani kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025.
Mwenyekiti wa Umoja wa Waendesha Bodaboda Mkoa wa Mwanza, Mohamed Idd akihamasisha wananchi kushiriki kwa amani Uchaguzi Mkuu 2025.
Mlezi wa makundi maalum Nyamagana, Stanslaus Mabula akihimiza wananchi kushiriki kwa amani Uchaguzi Mkuu 2025.
Mlezi wa makundi maalum Nyamagana, Stanslaus Mabula akihimiza wananchi kushiriki kwa amani Uchaguzi Mkuu 2025.
Mlezi wa makundi maalum Nyamagana, Stanslaus Mabula akihimiza wananchi kushiriki kwa amani Uchaguzi Mkuu 2025.
Makundi mbalimbali ikiwemo bodaboda wakiwa kwenye kongamano la kuhamasisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, Oktoba 29, 2025.
Makundi mbalimbali ikiwemo bodaboda wakiwa kwenye kongamano la kuhamasisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, Oktoba 29, 2025.
Bodaboda wakitoka uwanja wa Nyamagana baada ya kongamano la kuhamasisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, Oktoba 29, 2025.






No comments: