MBUNGE WA ILEMELA ASAFIRISHWA KWENDA INDIA KWA AJILI YA MATIBABU.
Hayo yalibainishwa jana na
Mbunge wa Jimbo la Nyamagana (Chadema) Ezekiel Wenje katika Mkutano wa hadhara wa Chadema uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mbugani Jijini Mwanza, ambao pia ulihudhuriwa na viongozi wa Kitaifa wa Chama hicho.
"...Hali ya Mbunge wenu Higness Kiwia si nzuri na usiku wa leo tunamsafirisha kwenda nchini India kwa ajili ya Matibabu.Kwa muda mrefu Kiwia amekuwa akisumbuka kutokana na majeraha aliyoyapata baada ya kuvamiwa na kukatwa mapanga akiwa na wenzake ambapo baadhi ya mishipa yake ya usoni ilikatwa hali ambayo imesababishia ganzi katika uso wake kiasi kwamba hivi sasa hata ukimpiga ngumi hasikii chochote..." Alisema Wenje huku akiwataka wapiga kura wake kumuombea ili apate ahueni kwa jili ya kurejea ili aendelee kuwatumikia.
Wenje aliongeza kuwa kwa muda mrefu mbunge huyo amekuwa akisumbuliwa kutokana na majeraha aliyoyapata mwaka 2012 baada ya kuvamiwa na watu waliosadikiwa kutumwa kwa ajili ya kumuangamiza kutokana na itikadi zilizoelezwa kuwa ni za kisiasa akiwa na makada wengine wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema.
Wananchi wakiwa katika hali ya Utulivu wakiwasikiliza Viongozi wa Chadema waliokuwa wakihutubia katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika jana katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza. |
Walieleza kwamba kitendo cha Sitta kuliongoza Bunge hilo kufanya marekebisho ya Sheria za upigaji kura katika Bunge hilo kwa kuwaruhusu wajumbe watakaokuwa nje ya bunge kupiga kura, ni mbinu cha za kutafuta kura kwa namna yoyote ile kwa ajili ya kuhakikisha kwamba theluthi mbili ya kura za wajumbe wa bunge hilo kutoka pande zote mbili za bara na visiwani inapatikana.
Baadhi ya Viongozi wa Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA Mkoa wa Mwanza. Vyama hivyo ni Chadema, NCCR Mageuzi pamoja na CUF. |
Viongozi mbalimbali wa Chadema. |
Viongozi wa Chadema na CUF. |
Naibu Katibu Mkuu Chadema kutoka Tanzania Visiwani Salum Mwalimu. |
Naibu Katibu Mkuu Chadema Tanzania Bara John Mnyika. |
Mbunge wa Jimbo la Nyamagana (Chadema) Ezekiel Wenje (Alienyoosha Mkono juu). |
No comments: