Picha ya Pamoja baina ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Viongozi wengine akiwemo Meya wa Jiji la Mwanza, Uongozi wa Kiwanda cha Pespi SBC Tanzania, Shirika la EBLI na baadhi ya wanafunzi waliochishwa Masomo Mkoani Mwanza kutokana na sababu mbalimbali ikwemo mimba.
Baadhi ya wasichana walioachisha
masomo Mkoani Mwanza kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo Mimba, wamepatiwa
Vifaa vya biashara na Kampuni ya Vinywa ya Pepsi SBC Tanzania kwa lengo la
kuwasaidia wasichana katika shughuli zao za ujasiriamali.
Takribani
wasichana
45 Mkoani Mwanza wamenufaika na Vifaa hivyo ambavyo ni Matoroli
na Makasha ya kubebea barafu yaliyotolewa kwa akina dada 25, sanjari na meza
pamoja na viti kwa ajili ya akina dada 20 ambao tayari wameanzisha biashara ya
mama lishe.
Akikabidhi
vifaa hivyo jana, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo, alielezea
kufurahishwa na Msaada uliotolewa na Kampuni hiyo ya Vinywaji ya Pepsi SBC Tanzania
kwa kuwa utawawezesha wasichana hao kuboresha biashara zao.
“Vifaa hivi
ni imani yangu kuwa vitaboresha biashara za akina dada hawa na hivyo
kuwaongezea tija katika uendeshaji wa shughuli zao na kuongeza kipato chao
kiuchumi”. Alisema Mhandisi Ndikilo.
Katika hatua
nyingine Mhandisi Ndikilo amelishukuru Shirika lisilo la Kiserikali Mkoani
Mwanza la Education for Better Living (EBLI) ambalo kwa kushirikiana na wadau
wengine kama Pespi SBC Tanzania limeadhimia kuwasaidia wasichana walioacha
masomo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo suala la Miamba.
|
No comments: